ABN News

ABN News Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ABN News, Media/News Company, 14300 Cornerstone Village Drive Ste 126, Houston, TX.

03/01/2026

Global Adventist Church News Highlights
Top story:-SDA Tanzania Board of Trustees Dissolved

02/08/2026

Global Adventist Church News Highlights.
Top story: Sunday Laws Proposal Sparks Serious Religious Liberty Concerns

12/28/2025

Tanzania yapata chaneli Mpya ya Habari kwa Viwango vya Kimataifa!!
# 🇹🇿 🇰🇪

12/21/2025

Global Adventist Church News Highlights.

Polisi Wavunja Mtandao wa Usafirishaji Haramu wa Wakenya Kupelekwa Kupigana Nchini UkrainePolisi nchini Kenya wamewaokoa...
09/29/2025

Polisi Wavunja Mtandao wa Usafirishaji Haramu wa Wakenya Kupelekwa Kupigana Nchini Ukraine

Polisi nchini Kenya wamewaokoa zaidi ya watu 20 kutoka kwa mtandao unaoshukiwa wa usafirishaji haramu wa binadamu, uliodaiwa kuwadanganya wakenya waliotafuta ajira kwa ahadi za kazi nchini Urusi, kisha kuwatuma kupigana vitani nchini Ukraine.

Operesheni hiyo ilifanyika kufuatia msako ulioongozwa na taarifa za kijasusi katika eneo la Athi River, viunga vya jiji la Nairobi, ambapo maafisa walik**ata nyaraka za usajili, hati za kusafiria na barua bandia za ofa za kazi.

Mshukiwa mmoja, anayedaiwa kuratibu safari za wahanga mwezi Septemba na Oktoba, amek**atwa na mahak**a ya Nairobi imeruhusu polisi kumzuilia kwa siku 10 ili kukamilisha uchunguzi.

Mamlaka zinasema mtandao huo umekuwa ukiwatoza wakenya fedha nyingi kwa ahadi za kazi zenye malipo makubwa jijini Moscow. Badala yake, wahanga walifichua kuwa walilazimishwa kusaini mikataba iliyowataka kulipa hadi dola 18,000 (takriban shilingi milioni 2.3) kwa ajili ya visa, usafiri, malazi na gharama nyingine. Baadhi yao walikuwa tayari wamelipa malipo ya awali ya dola 1,500.

Polisi walithibitisha kuwa jumla ya Wakenya 22 walipatikana katika nyumba moja eneo la Athi River “wakisubiri kusafirishwa kwenda Urusi.” Uchunguzi unaonyesha mpango wa mwisho ulikuwa ni kuwatuma vitani Ukraine kupigania upande wa Urusi.

Kumekuwa na ongezeko la wasiwasi kuhusu idadi kubwa ya Wakenya wanaosafirishwa nje kwa ahadi za uongo za ajira. Hivi karibuni, mwanariadha kijana wa Kenya alik**atwa nchini Ukraine, akidai alidanganywa kujiunga na jeshi la Urusi. “Mimi ni Mkenya, msinipige risasi,” alisema baada ya kudanganywa kuingia vitani.

Maafisa wanasema wengi wa wanaosafirishwa hurudi nyumbani wakiwa wamejeruhiwa, wameathirika kisaikolojia, au wengine hawarudi kabisa. Wakenya wawili wamerejeshwa hivi karibuni, mmoja wao akiwa amelazwa katika hospitali moja jijini Nairobi.

Wizara ya Mambo ya Nje imethibitisha kuwa inafuatilia taarifa za Wakenya kadhaa waliodaiwa kusafirishwa hadi Urusi na sasa wanashikiliwa k**a mateka wa vita nchini Ukraine.

Ripoti za kimataifa pia zinaonyesha kuwa raia wa Somalia, Sierra Leone, Togo, Cuba na Sri Lanka wako miongoni mwa walioko kwenye kambi za mateka wa vita nchini Ukraine. Msemaji wa Ukraine kuhusu masuala ya mateka wa vita, Petro Yatsenko, aliwahi kuiambia BBC kwamba “mataifa mengi ya Afrika hayaonyeshi nia ya kuwarudisha raia wao na hayapendi kuwapokea tena.”

Vijana Wawili Wa Kisomali Kortini kwa Kudhalilisha Bendera ya Kenya Uwanjani NyayoNairobi, Kenya – Septemba 26, 2025Vija...
09/26/2025

Vijana Wawili Wa Kisomali Kortini kwa Kudhalilisha Bendera ya Kenya Uwanjani Nyayo

Nairobi, Kenya – Septemba 26, 2025

Vijana wawili raia wa Somalia wamefikishwa katika Mahak**a ya Milimani wakikabiliwa na shtaka la kudhalilisha bendera ya taifa la Kenya wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League) iliyochezewa Uwanja wa Nyayo.

Vijana hao, wenye umri kati ya miaka 14 na 17, walifika mbele ya Hakimu Mkuu Mwandamizi Rose Gitau katika Mahak**a ya Watoto siku ya Ijumaa wakiwa chini ya ulinzi mkali.

Kuk**atwa kwao kulitokana na kusambaa kwa video mtandaoni mnamo Septemba 20, ikionyesha mashabiki wakikosea heshima bendera ya Kenya wakati wa pambano kati ya Mogadishu City Club na Kenya Police FC. Katika video hiyo, mashabiki walionekana wakikanyaga, kuipiga teke na kuitupa bendera hiyo. Mshabiki mmoja alionekana akiipangusa sehemu zake za siri, huku mwingine aliyevaa kikoi cha Kisomali akinyakua bendera kutoka kwa shabiki wa Police FC na kuirusha chini.

Video hiyo ilizua hasira kubwa miongoni mwa Wakenya, na kusababisha uchunguzi uliopelekea kuk**atwa kwa haraka kwa washukiwa.

Waziri wa Usalama wa Ndani, Kipchumba Murkomen, alilaani kitendo hicho akikitaja kuwa “cha kusikitisha” na akaonya kwamba wageni watakaopatikana na hatia watafukuzwa nchini pamoja na kufikishwa mahak**ani.
“Hatuwezi kuruhusu yeyote, awe raia au mgeni, kudhalilisha uhuru wetu na alama za umoja wetu,” Murkomen alisema katika kongamano la usalama mjini Wajir.

Balozi wa Somalia nchini Kenya, Jabril Ibrahim Abdulle, pia alijitenga na tukio hilo, akisisitiza kuwa halikuwa msimamo wa serikali ya Somalia.

Sheria ya National Flag, Emblems and Names Act (Sura ya 99) inakataza vitendo vya kudharau bendera ya taifa, wimbo wa taifa au alama zake, na inabainisha adhabu ya faini au kifungo cha hadi miezi sita.

Murkomen alionya kuwa Kenya haitavumilia wahalifu: “Kuwa nchini Kenya ni heshima. Ukidharau alama zetu za kitaifa, unahatarisha kupoteza heshima hiyo.”

Chakwera Akubali Matokeo, Ampongeza Mutharika kwa Ushindi wa Urais MalawiLilongwe, Malawi – Rais wa Malawi, Lazarus Chak...
09/24/2025

Chakwera Akubali Matokeo, Ampongeza Mutharika kwa Ushindi wa Urais Malawi

Lilongwe, Malawi – Rais wa Malawi, Lazarus Chakwera, ameungana na wananchi wa taifa hilo kushuhudia mabadiliko ya uongozi baada ya kukubali kushindwa katika uchaguzi wa urais uliofanyika Septemba 16.

Katika hotuba iliyotangazwa moja kwa moja kupitia televisheni, saa chache kabla ya Tume ya Uchaguzi ya Malawi kutangaza matokeo rasmi, Chakwera aliwashukuru Wamalawi kwa kumuunga mkono kwa kipindi cha miaka mitano aliyohudumu madarakani.

Alimpongeza mpinzani wake, Rais wa zamani Peter Mutharika, kwa ushindi wa kura zaidi ya milioni moja, akieleza kuwa tayari amempigia simu kumtakia kila la heri k**a Rais wa 7 wa Jamhuri ya Malawi.

Matokeo ya awali yanaonyesha Mutharika, mwenye umri wa miaka 85, akipata takribani asilimia 66 ya kura halali, huku Chakwera akipata asilimia 24 pekee.

Chakwera, aliyewahi kuchaguliwa mwaka 2020 baada ya Mahak**a ya Katiba kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa 2019, ataondoka madarakani huku taifa likikumbwa na changamoto za kiuchumi. Wakati huohuo, Mutharika anatarajiwa kurejea Ikulu akiahidi kuimarisha uchumi na kuendeleza miradi ya maendeleo aliyoanzisha awali.
🇲🇼🇲🇼🇲🇼

Holly Hagan-Blyth Afunguka Kuhusu Kupoteza Hamu ya Ngono Baada ya KujifunguaMwanamichezo na nyota wa televisheni ya uhal...
09/23/2025

Holly Hagan-Blyth Afunguka Kuhusu Kupoteza Hamu ya Ngono Baada ya Kujifungua

Mwanamichezo na nyota wa televisheni ya uhalisia, Holly Hagan-Blyth, amefichua kuwa alipoteza hamu ya ngono baada ya kujifungua mwanawe, Alpha-Jax, mwaka wa 2023 — changamoto ambayo anasema mama wengi wapya hukabiliana nayo kimya kimya.

Akizungumza katika CBeebies Parenting Helpline, Hagan-Blyth alisema hakuhisi hamu ya ukaribu wa kimwili na mumewe, Jacob, katika miezi baada ya kujifungua.

“Ningeweza kusema, ‘sikiliza, k**a hunitaki tena, sina shida,’ kwa sababu ndivyo nilivyohisi wakati huo,” alikiri.

Alieleza kuwa hata ishara ndogo za mapenzi k**a kukumbatiana zilimfanya ahisi shinikizo la tendo la ndoa, jambo ambalo hakuwa tayari nalo. “Nilianza kuhusisha vibaya hata kitendo cha kumgusa au kumkumbatia,” alisema.

Hata hivyo, alisema kuwa ukweli na mawasiliano ya moja kwa moja na mumewe yalisaidia kuondoa shinikizo hilo.

Jacob, kwa upande wake, awali aliogopa kuwa mkewe hampendi tena. “Nilimwambia kuwa hili halina uhusiano wowote na wewe,” Hagan-Blyth alisema. “Sihisi kufanya ngono kwa sasa, au hata katika miezi michache ijayo. Hili ni jambo langu binafsi ambalo ninahitaji kulipitia.”

Wataalamu wanasema hali hiyo ni ya kawaida. Mtaalamu wa mahusiano na ngono, Rachel Gold, alisema wanandoa wengi hukosea kudhani kuwa ukaribu lazima urudi baada ya uchunguzi wa wiki sita wa baada ya kujifungua. “Hiyo inawafanya wengi kuamini lazima waanze tendo la ndoa tena, lakini si kweli,” alisema.

Daktari bingwa wa uzazi na magonjwa ya wanawake, Jennifer Lincoln, alieleza kuwa mabadiliko ya homoni, uchungu wa mwili, na mchakato wa kupona huchangia kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa. “Siku chache baada ya kujifungua huleta mabadiliko makubwa zaidi ya homoni ambayo mwanamke atawahi kupitia,” alisema.

Changamoto hii haikumbi wanawake pekee. Mskilizaji mmoja wa CBeebies, Frankie, alisema mwenzi wake alipoteza hamu ya ngono baada ya kupata mtoto wao. “Ninachukia mwili wangu kwa sasa, na ninataka tu kupata upendo zaidi kutoka kwa mwenzi wangu, lakini hataki tena kufanya ngono nami. Ninahisi kukwama,” alieleza.

Wataalamu wanasema wanaume pia hukabiliana na changamoto za kisaikolojia baada ya kuwa baba, ingawa mara nyingi hali zao hupuuzwa. Fleur Parker kutoka shirika la National Childbirth Trust alihimiza wanandoa kuzungumza waziwazi: “Usidhani mwenzi wako anajua unachohisi au unachofikiria.”

Hagan-Blyth anatumaini uwazi wake utahamasisha wanandoa wengine kuzungumzia masuala ya ukaribu baada ya kujifungua. “Watu husema uhusiano hubadilika baada ya kupata mtoto, lakini hadi ufike pale ndipo unatambua ukubwa wa mabadiliko hayo,” alisema.

Wataalamu wanashauri wanandoa kutafuta msaada wa kitaalamu iwapo changamoto za ukaribu zitazua mvutano. “Wazazi wapya wengine hujipanga upya kwa urahisi, lakini wengine hupata msongo mkubwa wa mawazo,” Dkt. Lincoln alisema. “Iwapo inaleta mgogoro mkubwa wa kifamilia, ushauri wa kitaalamu unaweza kusaidia sana.”

“Familia Yateseka: Wazazi wa Afisa wa Polisi Aliyepotea Haiti Wadai Majibu Kabla ya Kesi Kusikizwa”Familia ya afisa wa p...
09/18/2025

“Familia Yateseka: Wazazi wa Afisa wa Polisi Aliyepotea Haiti Wadai Majibu Kabla ya Kesi Kusikizwa”

Familia ya afisa wa polisi wa Kenya aliyeendelea kutoweka wakati wa jukumu la kulinda amani nchini Haiti inaitaka serikali kutoa majibu ya haraka kuhusu aliko, huku mashaka juu ya hatima yake yakiendelea kuwatesa.

Kwenye kikao cha mtandaoni cha Mahak**a ya Milimani siku ya Alhamisi, Wakili Mwandamizi Mbuthi Gathenji, anayewakilisha mama ya afisa huyo, Jacinta Wanjiku Kabiru, pamoja na jamaa wengine, alipinga ombi la upande wa Serikali la kuahirisha kesi hiyo.

Afisa huyo, Benedict Kabiru Kuria, aliripotiwa kupotea mwezi Machi baada ya msafara wa Wakenya chini ya jukumu la Multinational Security Support (MSS) kushambuliwa na magenge yenye silaha nchini Haiti.

Wakili wa Serikali, Betty Mwasao, akiwakilisha Mwanasheria Mkuu, Inspekta Jenerali wa Polisi na mashirika mengine, aliomba kuahirishwa kwa kesi, akisema alikuwa akihudumia mteja hospitalini na pia alikuwa mapumzikoni. Lakini Gathenji alikataa hoja hiyo, akieleza kuwa familia imevumilia “miezi ya kimya cha kuumiza moyo” bila taarifa yoyote juu ya mwana wao aliyepotea.

“Mleta maombi amekuwa akisubiri taarifa juu ya mwanawe mwenyewe, afisa aliyepotea Haiti. Naomba tuisikize kesi leo,” Gathenji aliomba mahak**ani.

Jaji wa Mahak**a Kuu, Chacha Mwita, aliwasihi jamaa wawe na subira, akisisitiza umuhimu wa kusawazisha haki ya familia kupata majibu kwa wakati na wajibu wa serikali kukusanya taarifa sahihi. Mahak**a ilipanga Septemba 24 saa 5:30 asubuhi kusikilizwa kwa kesi hiyo kwa hadhara.

Familia hiyo iliwasilisha ombi lao mwezi Julai chini ya cheti cha dharura, wakitaka mahak**a iamuru mashirika ya serikali—ikiwemo Wizara ya Mambo ya Nje na ya Ndani—kuthibitisha k**a Kuria bado yuko hai au amekufa, na kufichua hatua zote zilizochukuliwa kumtafuta.

Pia waliomba serikali iwezeshe mawasiliano ya moja kwa moja na familia.

Inspekta Jenerali Douglas Kanja hapo awali alikiri kwamba kuna afisa mwingine wa Kenya ambaye bado hajapatikana nchini Haiti, akisema juhudi za kuwapata zinaendelea. Ripoti zinaonyesha msafara huo ulivamiwa walipokuwa wakisaidia gari la polisi wa Haiti lililokwama mtaroni, shimo linaloshukiwa kuchimbwa na magenge.

Kwa Wanjiku na familia yake, mateso ya kusubiri yanaendelea. Ombi lao kwa serikali ni moja na lenye kugusa moyo:
“Tuambieni mtoto wetu yuko wapi.”

Faith Kipyegon Aibuka Mshindi wa Dhahabu ya Kihistoria ya Dunia ya 1500m kwa Mara ya NneMkenya Faith Kipyegon amejiimari...
09/16/2025

Faith Kipyegon Aibuka Mshindi wa Dhahabu ya Kihistoria ya Dunia ya 1500m kwa Mara ya Nne

Mkenya Faith Kipyegon amejiimarisha k**a mmoja wa wakimbiaji bora zaidi wa mbio za kati baada ya kushinda taji la dunia la 1500m kwa mara ya nne nchini Japani.

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 31 alidhibiti mbio kuanzia mwanzo hadi mwisho, kisha akatumia kasi yake ya kipekee katika mzunguko wa mwisho kumaliza kwa muda wa 3:52.15. Ushindi huo ulimwezesha Kenya kushinda medali mbili baada ya Dorcus Ewoi kushika nafasi ya pili, huku Jessica Hull wa Australia akibeba nishani ya shaba.

Kipyegon sasa ameungana na nguli wa Morocco aliyestaafu, Hicham El Guerrouj, k**a wanariadha pekee katika historia kushinda mataji manne ya dunia katika mbio hizo. Pia amefikisha jumla ya medali za dhahabu nane za kimataifa, sawa na bingwa wa mbio fupi wa Jamaica Shelly-Ann Fraser-Pryce na nyota wa Ethiopia Tirunesh Dibaba, ambao wote wamewahi kushinda idadi hiyo katika mashindano ya kimataifa ya mtu mmoja mmoja.

Baada ya ushindi huo, Kipyegon alisema kwa furaha:

“Ninamshukuru Mungu. Nilijua ninaweza kutetea taji langu baada ya kuvunja rekodi ya dunia mapema mwaka huu. Nilichotaka tu ni kukimbia kwa utulivu bila kusukumana au kuanguka. Nilihitaji kuwa peke yangu na kukimbia mbio zangu.”

Akiwa hajaangushwa katika fainali tano za kimataifa mfululizo, na bila kupoteza katika 1500m kwa zaidi ya miaka minne, Kipyegon anaendelea kutawala mbio hizi zinazochukuliwa kuwa na ushindani mkubwa. Kasi yake ya mwisho isiyolinganishwa imewaacha wapinzani wake wakifuatia tu, huku ni Sifan Hassan pekee aliyewahi kumzima tangu mwaka 2017.

Kipyegon, ambaye alitengeneza historia miaka miwili iliyopita kwa kuwa mwanamke wa kwanza kushinda mataji ya dunia ya 1500m na 5000m kwa pamoja, sasa analenga kurudia mafanikio hayo wakati mchujo wa 5000m utakapoanza wiki hii.

Kutoka kukimbia peku akienda shule kijijini kwao hadi kuweka rekodi kwenye jukwaa la dunia, safari ya Kipyegon ni ya uvumilivu, ubabe, na msukumo. Anaendelea kuvunja mipaka, hivi majuzi akijaribu kuwa mwanamke wa kwanza kukimbia maili chini ya dakika nne — ingawa hakufanikisha, bado aliweka rekodi mpya ya dunia yake mwenyewe.

Ushindi wake, sawa na ule wa nyota wa kuruka kijiti Armand Duplantis, unaonyesha dalili chache za kusimama. K**a alivyosema mchambuzi Andrew Cotter:

“Anafanya mzunguko wa tatu uwe wa kasi kuliko wa pili, na wa pili uwe wa haraka kuliko wa kwanza. Hii inamaanisha hakuna mwingine anayeweza kufanya chochote ila kustahimili na kushikilia."

Mwanamke Ak**atwa kwa Tuhuma za Kumchoma Kisu Mumewe Hadi Kufa Kitengela- KenyaKitengela, Kaunti ya Kajiado – Polisi mji...
09/15/2025

Mwanamke Ak**atwa kwa Tuhuma za Kumchoma Kisu Mumewe Hadi Kufa Kitengela- Kenya

Kitengela, Kaunti ya Kajiado – Polisi mjini Kitengela wamemk**ata mwanamke mwenye umri wa miaka 24 kwa madai ya kumchoma kisu mumewe wa miaka 38 hadi kufa usiku wa Jumapili.

Marehemu alikimbizwa Hospitali ya Kitengela Subcounty na majirani, lakini madaktari walimthibitisha kuwa amefariki alipowasili. Ripoti za polisi zinasema alifariki kutokana na kutokwa damu nyingi baada ya kuchomwa kwenye paja, akidaiwa kuchomwa na mkewe ambaye wameishi naye kwa miaka miwili.

Kisu cha jikoni kilichokuwa na damu kilipatikana ndani ya nyumba yao ya kupangisha na kimehifadhiwa k**a ushahidi. Mshukiwa amezuiliwa katika kituo cha polisi Kitengela na anatarajiwa kufikishwa katika Mahak**a ya Kajiado Jumanne, akikabiliwa na shtaka la mauaji.

Polisi wanasema mwanamke huyo alimwapigia simu baba mkwe wake majira ya saa mbili na nusu usiku na kukiri kwamba alichoma kisu mumewe. Kwa msaada wa majirani, walimkimbiza hospitalini, lakini alifariki kutokana na kuvuja damu kupita kiasi.

Baba wa marehemu amesema hii si mara ya kwanza mwanawe kujeruhiwa na mkewe, akieleza ndoa yao k**a yenye vurugu nyingi. Anadai mshukiwa alimshambulia mwanawe mara kadhaa hapo awali, ikiwemo kumpiga kisu kifuani na kumshambulia akiwa nyumbani kwake.

“Ndoa yao ilikuwa ya vurugu. Hii si mara ya kwanza. Kuna visa vingine ambapo mshukiwa alimchoma kisu kifuani, na nyingine alipomshambulia nyumbani kwangu,” alisema.

Siku ya tukio, marehemu alihudhuria ibada ya kanisa pamoja na baba yake kabla ya kuelekea nyumbani kwake eneo la Orata, Kitengela, ambako alikutana na mauti.

Maafisa wa upelelezi wa DCI kutoka kituo cha polisi Kitengela wameanzisha uchunguzi wa tukio hilo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Kitengela Subcounty ukisubiri kufanyiwa upasuaji wa maiti.

Address

14300 Cornerstone Village Drive Ste 126
Houston, TX
77014

Opening Hours

Monday 9am - 5pm
Tuesday 9am - 5pm
Wednesday 9am - 5pm
Thursday 9am - 5pm
Friday 9am - 5pm
Sunday 9am - 5pm

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ABN News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to ABN News:

Share