09/23/2025
Holly Hagan-Blyth Afunguka Kuhusu Kupoteza Hamu ya Ngono Baada ya Kujifungua
Mwanamichezo na nyota wa televisheni ya uhalisia, Holly Hagan-Blyth, amefichua kuwa alipoteza hamu ya ngono baada ya kujifungua mwanawe, Alpha-Jax, mwaka wa 2023 — changamoto ambayo anasema mama wengi wapya hukabiliana nayo kimya kimya.
Akizungumza katika CBeebies Parenting Helpline, Hagan-Blyth alisema hakuhisi hamu ya ukaribu wa kimwili na mumewe, Jacob, katika miezi baada ya kujifungua.
“Ningeweza kusema, ‘sikiliza, k**a hunitaki tena, sina shida,’ kwa sababu ndivyo nilivyohisi wakati huo,” alikiri.
Alieleza kuwa hata ishara ndogo za mapenzi k**a kukumbatiana zilimfanya ahisi shinikizo la tendo la ndoa, jambo ambalo hakuwa tayari nalo. “Nilianza kuhusisha vibaya hata kitendo cha kumgusa au kumkumbatia,” alisema.
Hata hivyo, alisema kuwa ukweli na mawasiliano ya moja kwa moja na mumewe yalisaidia kuondoa shinikizo hilo.
Jacob, kwa upande wake, awali aliogopa kuwa mkewe hampendi tena. “Nilimwambia kuwa hili halina uhusiano wowote na wewe,” Hagan-Blyth alisema. “Sihisi kufanya ngono kwa sasa, au hata katika miezi michache ijayo. Hili ni jambo langu binafsi ambalo ninahitaji kulipitia.”
Wataalamu wanasema hali hiyo ni ya kawaida. Mtaalamu wa mahusiano na ngono, Rachel Gold, alisema wanandoa wengi hukosea kudhani kuwa ukaribu lazima urudi baada ya uchunguzi wa wiki sita wa baada ya kujifungua. “Hiyo inawafanya wengi kuamini lazima waanze tendo la ndoa tena, lakini si kweli,” alisema.
Daktari bingwa wa uzazi na magonjwa ya wanawake, Jennifer Lincoln, alieleza kuwa mabadiliko ya homoni, uchungu wa mwili, na mchakato wa kupona huchangia kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa. “Siku chache baada ya kujifungua huleta mabadiliko makubwa zaidi ya homoni ambayo mwanamke atawahi kupitia,” alisema.
Changamoto hii haikumbi wanawake pekee. Mskilizaji mmoja wa CBeebies, Frankie, alisema mwenzi wake alipoteza hamu ya ngono baada ya kupata mtoto wao. “Ninachukia mwili wangu kwa sasa, na ninataka tu kupata upendo zaidi kutoka kwa mwenzi wangu, lakini hataki tena kufanya ngono nami. Ninahisi kukwama,” alieleza.
Wataalamu wanasema wanaume pia hukabiliana na changamoto za kisaikolojia baada ya kuwa baba, ingawa mara nyingi hali zao hupuuzwa. Fleur Parker kutoka shirika la National Childbirth Trust alihimiza wanandoa kuzungumza waziwazi: “Usidhani mwenzi wako anajua unachohisi au unachofikiria.”
Hagan-Blyth anatumaini uwazi wake utahamasisha wanandoa wengine kuzungumzia masuala ya ukaribu baada ya kujifungua. “Watu husema uhusiano hubadilika baada ya kupata mtoto, lakini hadi ufike pale ndipo unatambua ukubwa wa mabadiliko hayo,” alisema.
Wataalamu wanashauri wanandoa kutafuta msaada wa kitaalamu iwapo changamoto za ukaribu zitazua mvutano. “Wazazi wapya wengine hujipanga upya kwa urahisi, lakini wengine hupata msongo mkubwa wa mawazo,” Dkt. Lincoln alisema. “Iwapo inaleta mgogoro mkubwa wa kifamilia, ushauri wa kitaalamu unaweza kusaidia sana.”