Marianna Ciera

Marianna Ciera The content provided is taken from user submitted content. This page is not part of the official Reddit. East African Leading source for Infotainment News

Kwa mujibu wa taarifa za awali zinasema kuwa sababu zilizopelekea Ndege ya Air India kudondoka mwezi Juni 12, 2025 na ku...
07/12/2025

Kwa mujibu wa taarifa za awali zinasema kuwa sababu zilizopelekea Ndege ya Air India kudondoka mwezi Juni 12, 2025 na kuua watu 260 ilitokana na kuzimwa kwa mafuta ya Injini zote mbili za Ndege.

Kwa mujibu wa sauti za Marubani wa Ndege hiyo zilizorekodiwa kwenye Black Box alisikika Rubani mmoja akimuuliza Rubani mwenzake kuwa, "Kwanini umezima mafuta kwenye Injini?, Rubani mwenzake akamjibu Sijafanya hivyo,". Sekunde kadhaa Ndege ikadondoka.

Kwa wapenzi wa movie, series na hasa mashabiki wa Squid Game, kuna habari njema.Mtayarishaji wa Squid Game, Hwang Dong-h...
07/11/2025

Kwa wapenzi wa movie, series na hasa mashabiki wa Squid Game, kuna habari njema.

Mtayarishaji wa Squid Game, Hwang Dong-hyuk, amesema kuwa japokuwa msimu wa 3 utahitimisha baadhi ya sehemu za hadithi, bado hajafunga milango ya kuendelea na msimu wa 4.

Hii ina maana kuwa Squid Game huenda ikaendelea zaidi ya msimu wa 3, na kuna uwezekano mkubwa wa kuona vipindi vingine vya mfululizo (spin-offs), k**a vile toleo la Marekani, au hata mwelekeo mpya kabisa endapo wazo litakaa vizuri.

Klabu ya Liverpool imeamua kuistaafisha jezi namba 20 iliyokuwa inavaliwa na mshambuliaji Diogo Jota aliyepoteza maisha ...
07/11/2025

Klabu ya Liverpool imeamua kuistaafisha jezi namba 20 iliyokuwa inavaliwa na mshambuliaji Diogo Jota aliyepoteza maisha Julai 03, 2025 kwa ajali ya gari huko Uhispania ambapo jezi hiyo haitavaliwa na mchezaji yeyote kwenye madaraja yote ya klabu hiyo.

Jota na kaka yake, Andre Silva, walipoteza maisha kwenye ajali ya gari huko Uhispania mnamo Julai 3, 2025 huku majogoo hao wakipanga kuutumia mchezo wa Jumapili dhidi ya Preston kwa ajili ya kumuenzi nyota huyo raia wa Ureno.

Wanasayansi wanaamini kuwa kuna bahari kubwa iliyojificha chini ya uso wa sayari yaMars, imefunikwa na miamba kwa kina k...
07/11/2025

Wanasayansi wanaamini kuwa kuna bahari kubwa iliyojificha chini ya uso wa sayari ya
Mars, imefunikwa na miamba kwa kina kirefu.

Taarifa kutoka kwa kifaa cha NASA kiitwacho InSight zinaonyesha kuwa maji hayo huenda yana chumvi nyingi kiasi cha kuendelea kuwa katika hali ya kimiminika hata k**a kuna baridi kali.

Hii ina maana kuwa huenda Mars bado ina mazingira yanayoweza kuhimili aina fulani ya uhai, hasa wa vijidudu vidogo. Sayari hiyo nyekundu, ambayo kwa muda mrefu tumedhani kuwa ni kavu na tupu, huenda ina mambo mengi yaliyofichika chini ya uso wake.

Marioo ameachia video ya wimbo wake wa   muda mchache uliopita ambapo mwanzoni  mwa video hiyo ameonekana akivishwa Taji...
07/11/2025

Marioo ameachia video ya wimbo wake wa muda mchache uliopita ambapo mwanzoni mwa video hiyo ameonekana akivishwa Taji la Kifalme (Crown) akiashiria ni rasmi yeye ndio MFALME wa kizazi kipya cha Bongofleva.

Je ni muda sasa wa Marioo kupewa hadhi hiyo⁉️ Tuambie.. 🤔

06/26/2025

Address

2710 S Huron Road
Kawkawlin, MI
48631

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Marianna Ciera posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Marianna Ciera:

Share