08/07/2025
Miezi miwili imepita tangu msanii Lava Lava aondoke kwenye lebo ya WCB, lebo iliyomtambulisha kwenye ulimwengu wa Bongo Fleva. Tangu kuondoka kwake, Lava Lava hajawahi kuchapisha chochote kuhusu maisha yake binafsi au kazi yake ya muziki kwenye mitandao ya kijamii, hali iliyowafanya mashabiki wake wajiulize maswali mengi.
Hata hivyo, kuna dalili zinazoonyesha kwamba huenda msanii huyo anajiandaa kuachia jambo jipya. Tumegundua kwamba amebadili picha yake ya wasifu (profile picture) kwenye Instagram. Picha hiyo mpya ina rangi ya bluu iliyokolea, rangi ya bluu iliyofifia, na nyeupe, picha k**a hiyo pia ameiweka kwenye InstaStory.
Mabadiliko haya madogo lakini ya maana yamefanya tujiulize: Je, hii ni ishara kwamba Lava Lava anajiandaa kutoa wimbo EP au albamu mpya?
Wewe mdau wa Bongo Fleva unafikiriaje?