IMELA SHOW

IMELA  SHOW Imelashow is a gospel show which brings together all its audience together as a family.

  is a gospel show which bring together all its funs and other people together as a family. IMELA means thank you God i therefore invite you for this wonderful show every Sunday from 7pm to 10pm.

Nasikia kuongea na mtu mmoja siku ya leo, sijui unapitia jaribu gani, sijui unapita kwenye changamoto gani, sijui kiwang...
15/07/2025

Nasikia kuongea na mtu mmoja siku ya leo, sijui unapitia jaribu gani, sijui unapita kwenye changamoto gani, sijui kiwango cha maumivu ulichonacho moyoni

Bwana amenipa Neno kwa ajili yako siku ya leo kwamba hakuna hali ambayo huwa inadumu katika maisha, hakuna uadui ambao huwa unadumu kila chenye mwanzo huwa kina mwisho

Nimetumwa kukwambia acha kujipa stress juu ya hali unayoipitia amini tu kwamba hata hilo utalishinda tu kwasababu unae mtetezi ambae ni Yesu Kristo atakutetea na kukushindia

Biblia inasema
Zaburi 23:4
Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti
Sitaogopa mabaya
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

Kila mwanadamu kuna wakati ambao lazima anapenda hapendi atapita kwenye bonde la uvuli wa mauti. Mahali ambapo tumaini linapotea, giza linatanda kila mahali

Lakini cha kutia moyo ni hiki kwamba kwenye bonde la uvuli wa mauti sio mahali tunakaa ni mahali tunapita. Nimetumwa kukwambia unapita tu wala hutakaa kwenye hiyo hali

Lakini pia pia Biblia inasema sitaogopa mabaya kwa maana Bwana yupo pamoja na wewe . Hata iweje, hata vita yako iwe kubwa kiasi gani, hata pito lako liwe kubwa kiasi gani hakikisha hauogopi
Sio kwamba maumivu hayatakuwepo yatakuwepo ila hakikisha hauogopi kwa maana Bwana yupo pamoja na wewe, Gongo lake na fimbo yake vitakufariji

13/07/2025

Wewe, Bwana, ndiwe wachuae siri ya machozi yangu. Katika dunia iliyojaa kelele, machozi yasiyoeleweka kwa watu, yapo machozi anayoyajua Bwana pekee.
🗓️ Jumapili | 7am–9am
🎙️ Sifa za Asubuhi na Kevin Keitany

13/07/2025

Tunatoa shukrani si kwa sababu sisi ni wakamilifu. Bali kwa sababu Yeye alitupenda hata kabla hatujamjua.
1 Yohana 4:19 Sisi twampenda, kwa kuwa yeye alitupenda kwanza

13/07/2025

🌅 Sunday Evenings Hit Different with 🙌
Join Kevin Keitany from 6PM–9PM for pure worship, thanksgiving, and testimonies za neema ya Mungu Tufuate online kwenye link: http://stream.zeno.fm/hmwhu0czetbvv

06/07/2025
13/04/2025

Leo ni Jumapili ya Mtende, siku ambayo Wakristo duniani hukumbuka kwa shangwe kuu kuingia kwa Yesu Kristo katika mji wa Yerusalemu.

Alikuja si kwa farasi wa kifalme, bali kwa mwana-punda — ishara ya unyenyekevu, amani, na upendo.
Watu walimtandika mavazi yao, wakamtupia matawi ya mitende njiani, wakisema kwa sauti kuu:
“Hosana! Abarikiwe ajaye kwa jina la Bwana!”

Lakini pia ni siku ya kutafakari.
Kwa sababu wale waliompokea kwa shangwe… baadaye wengine walipaza sauti zao wakisema, “Msulubishe!”
Ni ukumbusho kwetu kwamba mioyo ya watu hubadilika — lakini upendo wa Mungu hubaki thabiti.

Jumapili ya Mtende hutufundisha kuwa:
🕊️ Unyenyekevu ni nguvu, si udhaifu.
🕊️ Yesu anapokuja katika maisha yetu, si kwa kishindo cha dunia — bali kwa upole unaobadilisha ndani.
🕊️ Na kuwa na Yesu hakumaanishi kutembea bila dhiki, bali ni kuwa na amani hata katikati ya mateso.

Wiki Takatifu inaanza leo.
Ni safari ya kiroho kuelekea Msalabani — na hatimaye, kwenye tumaini la Ufufuo.
Hebu tujiandae, kimwili na kiroho. Tuwe tayari kupokea mfalme wa amani katika maisha yetu, familia zetu, na taifa letu.

16/02/2025

Kuna ahadi nyingi za Mungu katika Maandiko. Katika kila ahadi, Mungu anaahidi kwamba jambo fulani litafanyika (au halitafanyika) au litapeanwa au kutimia. Hizi sio ahadi duni, ahadi za kawaida k**a vile tunavyofanya mara nyingi; ahadi hizi za Mungu ni ahadi thabiti, ahadi zisizo na shaka zilizotolewa na Mungu mwenyewe. Kwa sababu Mungu ni mwaminifu

16/02/2025

Good morning na karibu kwenye kipindi hewani na Jumapili ya Baraka karibu tubarikiwe pamoja.
Tunajua Mungu anapenda kuwabariki watu. Hata anawapa mvua kwa wenye haki na wasio haki. Anapenda kubariki kadri anavyoweza. Baraka moja tunayopokea, kwa mfano, ni uvumilivu na subira yake – hata kuwapa wanadamu karne kadhaa wakati mwingine ili watubu kabla ya kuwahukumu, inajulikana sana. Anapenda kufanya mambo kwa watu. Mungu anapenda kubariki na KUWA baraka. Sasa fikiria hili: anasema pia anataka sisi tuwe k**a Yeye na anafanya iwezekane kupitia roho yake ndani yetu.

13/02/2025

It is and too karibu ndani ya kipindi hewani kuanzia 7.00pm hadi 10.00pm uweze kupata uhondo na burudani. Unawakilisha maeneo gani leo hii?.

09/02/2025

Good evening how was your Sunday, karibu ndani ya kipindi naye
tumshukuru Mungu kwa umbali huu ametufikisha, ni hapa ndani ya 99.9 Radio Domus Fm

14/07/2024

Kuujua Upendo wa Kristo Yesu alionyesha upendo wa kujidhabihu kwa njia bora sana. Kujidhabihu ni kutanguliza mahitaji na masilahi ya wengine bila ubinafsi.

14/07/2024

KUNA SIRI GANI KWENYE KUSIFU NA KUABUDU

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when IMELA SHOW posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to IMELA SHOW:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share