Serengeti Media Centre

  • Home
  • Serengeti Media Centre

Serengeti Media Centre Official Serengeti Media Centre page | FOLLOW Now | Media Activities and Production

Habari na Makala mbalimbali za Picha,Video na Sauti katika Nyanja za Kijamii,Siasa,Kiuchumi,Afya,Michezo na Burudani,Elimu na Matangazo.

Na Serengeti Media Centre - Seronera.Wanafunzi wanaolelewa na kupewa mafunzo ya elimu ya awali katika Kituo cha Michael ...
25/07/2025

Na Serengeti Media Centre - Seronera.

Wanafunzi wanaolelewa na kupewa mafunzo ya elimu ya awali katika Kituo cha Michael Academy kilichopo Mugumu Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara, leo Ijumaa Julai 25,2025 wamefanya ziara ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Wakiambatana na baadhi ya wazazi katika ziara hiyo ya siku moja imekuwa chachu kwa wanafunzi hao kufahamu na kuwaona wanyama sambamba na vivutio vya utalii wanavyojifunza kila siku darasani.

Endelea Kuwa Nasi katika kurasa na Channel yetu ya YouTube kufuatilia makala ya ziara hii.

24/07/2025

24/07/2025

TANZANIA YAPONGEZWA AFRIKA KUIDHINISHA MATIMIZI YA MBEGU ASILI KWA USALAMA WA CHAKULA.M***a Juma, Serengeti Media Centre...
24/07/2025

TANZANIA YAPONGEZWA AFRIKA KUIDHINISHA MATIMIZI YA MBEGU ASILI KWA USALAMA WA CHAKULA.

M***a Juma, Serengeti Media Centre -Ethiopia.

Serikali ya Tanzania imepongezwa kuwa ni miongoni mwa nchi chache barani Afrika,kupitisha mkakati wa kitaifa wa kuzitambua na kuzilinda mbegu za asili, ili kujihakikishia usalama wa chakula.

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe katika msimu wa mwaka 2024/25, ameidhinisha kusajiliwa matumizi ya mbegu 13 za asili za mazao mbali mbali ili zitumike na wakulima kwa mujibu wa sheria ya mbegu ya Tanzania, sura 308 kifungu cha 12(a) na 13(3).

Katika ufunguzi wa mkutano wa kujadili sera zinazoongoza mifumo ya chakula barani Afrika,Mratibu mkuu Shirika la kimataifa la Muungano wa Uhuru wa Chakula Afrika (AFSA) Dk.Million Belay na aliyekuwa Mwenyekiti wa K**ati ya bunge la Afrika Mashariki(EALA) ya kilimo, Utalii na Maliasili, Francoise Uwumukiza, walisema hatua ambayo imefikiwa na Tanzania na serikali ya Kenya kutambua mbegu za asili inafaa kuingwa na mataifa mengine.

Dk. Belay alisema ili bara la Afrika liwe na usalama wa chakula ni muhimu sana kuendeleza na kuzilinda mbegu za asili badala ya kutegemea mbegu za mazao mbali mbali kutoka nje ya Afrika.

"Bara la Afrika kwa miaka iliyopita lilikuwa ndio wazalishaji wakubwa wa chakula, kutokana na uwepo maarifa ya asili katika kilimo, lakini sasa limegeuka bara la kutegemea kila kitu kutoka nje ya Afrika zikiwepo mbegu za mazao"alisema

Dk.Belay alisema kutokana na mabadiliko ya tabia nchi yanayoendelea duniani na kulinda afya ya udongo, usalama wa chakula na baianuawai bara la Afrika linapaswa kuzilinda na kuzitumia mbegu zake za asili na kuendeleza kilimo Ikolojia.

Kwa upande wake, Mbunge wa EALA, Uwumukiza alisema Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, inatambua umuhimu wa mbegu za asili na inaunga mkono jitihada zilizofikiwa na serikali za Tanzania na Kenya kuanza kuzitambua mbegu hizo kwa kuzisajili.

Alisema utambuzi wa mbegu hizo ni utekelezaji wa miongozi ya Umoja wa nchi huru za Afrika, katika kulinda usalama wa chakula barani Afrika.

"EALA tutaendelea kutunga sera na sheria za kulinda mbegu za asili lakini tunaomba nchi nyingine barani Afrika nazo kuzitambua mbegu za asili na kuanza kuzilinda"alisema

Waziri wa Mipango na Maendeleo wa Ethiopia, Fitsum Assefa Adela alisema suala la usalama wa chakula barani Afrika ni muhimu kuendelea kujadiliwa na kuwekewa mikakati ya kudumu.

"Serikali ya Ethiopia inatambua umuhimu wa uwepo wa usalama wa chakula kwa ajili ya kulinda afya na watumiaji wa chakula lakini kujikinga pia na njaa"alisema

Kwa upande wake, Meneja miradi wa shirika la SIDA Afrika,Ayele Kebede Gebreyes, alisema shirika hilo kwa kushirikiana na mataifa mengine yataendelea kusaidia miradi ya kuhakikisha bara la Afrika linakuwa na usalama wa chakula.

Wakizungumzia hatua ya serikali ya Tanzania kuidhinisha matumizi ya mbegu za asili, Afisa miradi wa Shirikisho la wakulima Tanzania(SHIWAKUTA) ambaye pia ni Afisa miradi wa vikundi vya wakulima Arusha(MVIWAARUSHA) Damian James Sulumo alisema wanaishukuru serikali kuzitambua mbegu za asili.

"haikuwa kazi ndogo serikali kufikia uamuzi huu, tuliunda kikosi kazi cha masuala ya mbegu na kujadiliana na serikali na k**ati ya bunge la kilimo hadi kufikia makubaliano ambayo ni faraja kubwa kwetu"alisema

Sulumo alisema wizara ya kilimo, pia katika bajeti ya mwaka 2005/26 ilizungumzia umuhimu wa mbegu za asili na kuahidi kuendeleza tafiti zaidi ikiwepo ujenzi wa kituo maalum cha utafiti mkoani Arusha.

Afisa Ushawishi na utetezi wa SHIWAKUTA, Thomas Laizer alisema haiwezekani kuwa na mapinduzi ya kilimo kwa kutegemea mbegu kutoka nje ya Afrika na kuzitaja mbegu za asili zilizoidhinishwa Tanzania ni aina nne(4) ya mbegu za mahindi, Mpunga mbegu aina 4,mbegu za maharage aina mbili(2) na Papai aina tatu(3).

"Tanzania tumejaliwa kuwa na mbegu nyingi na nzuri za asili ambazo tunaamini zikitumika vizuri tutaongeza uzalishaji wa chakula lakini pia utakuwepo usalama wa chakula wakati wote na kuacha kutegemea mbegu kutoka nje ya nchi wakati wote" alisema.

Mkutano huo wa Usalama wa chakula unaendelea katika jiji la Addis Ababa ambapo nchi 23 barani Afrika zinashiriki, wakiwepo watafiti wa mazao, wataalam wa kilimo Ikolojia( Hai) wabunge, viongozi wa serikali, asasi za kiraia na waandishi wa habari.

24/07/2025

Na Serengeti Media - Mugumu, Serengeti.Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo imelipongeza Tamasha la Utalii wa Kiu...
23/07/2025

Na Serengeti Media - Mugumu, Serengeti.

Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo imelipongeza Tamasha la Utalii wa Kiutamaduni la Serengeti Cultural Festival linalofanyika kila mwaka wilayani Serengeti kwa kuwa chachu ya kukuza utalii na kudumisha mila na desturi za kitanzania kupitia sanaa za asili.

Akifungua tamasha hilo leo Julai 23,2025 katika viwanja vya Right to Play Mjini Mugumu Leah Kilimbi Mkurugenzi msaidizi wa Idara ya maendeleo ya sanaa kutoka wizara hiyo amesema kupitia tamasha hilo taifa limeweza kuonesha utamaduni wetu kwa wageni mbalimbali wa ndani na nje hususani wale wanaotembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

"Tunampongeza mratibu wa tamasha hili kwa kazi anayoifanya serikali inatambua jitihada zake, utamaduni ni roho ya taifa hivyo tutaendelea kutoa ushirikiano kadri inavyohitajika ili kuliboresha zaidi" amesema Leah.

Leah amewataka wasanii wanaofanya kazi za sanaa kuzirasimisha na kujisajiri katika Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ili waweze kupata urahisi wa kufanya kazi maeneo mbalimbali.

Joshua Nyansiri mratibu wa tamasha hilo amesema "ukitembelea hifadhi zetu kwa asilimia kubwa utamaduni wa kimaasai ndio unatambulika hivyo tumeamua kutoa kipaumbele kwa vikundi vya mkoa wetu ili viweze kuonesha walicho nacho na kukiuza nje" amesema Joshua na kuongeza,

"Nawakaribisha wadau na wananchi wote kutembelea katika maonesho haya ambayo yatafika tamati Julai 25 mwaka huu, zipo bidhaa nyingi za asili ni sehemu ya wewe kupata fursa ya kununua kwa bei rahisi sambamba na kutangaza bishara yako".

Endelea Kuwa Nasi
Zaidi Tazama YouTube Yetu

FURSA FURSA FURSA
23/07/2025

FURSA FURSA FURSA

M***a Juma,Addis AbabaSerengeti Media Centre.Waandishi wa Habari Barani Afrika wametakiwa kuwa na mtazamo chanya ili kuk...
23/07/2025

M***a Juma,Addis Ababa
Serengeti Media Centre.

Waandishi wa Habari Barani Afrika wametakiwa kuwa na mtazamo chanya ili kukuza kilimo Ikolojia kwa ajili ya Usalama na masoko ya chakula barani Afrika.

Kumekuwepo na ongezeko la uzalishaji na usambazaji wa vyakula ambavyo vimetokana na kilimo cha kemikali za viwandani na kupuuzwa kwa vyakula vinavyopatikana kwa mbegu za asili ya Afrika.

Chanzo ni mtizamo hasi kuwa
Kilimo Ikolojia hakina tija na ni cha kujikimu tu na hakiwezi kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya chakula jambo ambalo linapaswa kuelezwa kwa ukweli hasa ikizingatiwa kuwa kumekuwepo na athari za kiafya na kimazingira kutokana na matumizi ya mbegu,mbolea na viuatilifu vya viwandani.

Akifungua mafunzo hayo kwa wanahabari Afrika kuhusiana na Ujasiriamali wa Kilimo-Ikolojia Afrika na Masoko kwa ajili ya Uhuru wa Chakula Afrika yaliyoandaliwa Shirika la Alliance for Food Sovereignty in Africa (AFSA) Mratibu wa miradi wa Shirika hilo, Bridget Mugambe amesema, ni muhimu sana wanahabari barani Afrika kusaidia kuandika vizuri umuhimu wa kilimo Ikolojia Afrika.

Amesema, kumekuwepo na habari za kupotoshwa zisizo na ushahidi wa wazi juu ya mifumo ya kilimo Ikolojia ambacho, mizizi yake imejikita katika maarifa ya asili na uwezo wake wa kuleta manufaa ya kiafya, kiuchumi na kiikolojia.

"Mchango wa kilimo Ikolojia barani Afrika unaelezwa kuwa ni ndogo haustawi na hauchangii kikamilifu uchumi wa kisasa jambo ambalo sio kweli"alisema

Afisa mradi wa Masoko na Ujasiriamali wa AFSA Ruth Nabaggala amesema,wanahabari wanapaswa kupinga upotoshaji juu ya kilimo lkolojia na masoko yake kwa kuandika habari sahihi na zinazoinua hadhi ya uhuru wa chakula Afrika.

Kwa kuwa kuna ushahidi kutoka nchi za Ghana, Tunisia, na Zimbabwe unaoonesha kuwa biashara za kilimo-Ikolojia zinakidhi mahitaji halisi. Matunda na mboga ndizo bidhaa zinazotafutwa zaidi, zikifuatiwa na nafaka.

"Wateja wako tayari kuunga mkono mifumo hii kwa asilimia62 ya waliojibu utafiti walionesha utayari wa kulipa zaidi kwa bidhaa za kilimo-Ikolojia, na asilimia 53 wako tayari hata kufadhili wakulima kabla ya mavuno"amesema.

Hata hivyo amekiri, licha ya kuwepo na upotoshwaji bado pia hakuna sheria na sera rafiki za kuendeleza kilimo Ikolojia kwa nchi nyingi barani Afrika.

Kuhusiana na nafasi ya Ujasiriamali wa Kilimo Hai(Ikolojia) na Masoko katika kuleta Mageuzi ya Mfumo wa Chakula Afrika Dr Mamadou Goita amesema,soko la mazao ya chakula limedhibitiwa na makampuni makubwa kutoka nje ya Afrika.

Makampuni hayo ndio yanasambaza mbegu,mbolea na viatilifu na hivyo kudidimiza ukuaji wa kilimo Ikolojia licha ya umuhimu wake mkubwa kwa usalama wa chakula.

"K**a bara la Afrika linataka kuwa na usalama wa chakula lazima lihakikishe linauwezo wa kuzalisha na kusambaza mbegu na mazao yake ya asili ambayo kimsingi ni bora kuliko kutegemea kampuni za nje"alisema

Kwa kuwa mustakabali wa chakula Afrika unatakiwa kujikita katika kilimo endelevu cha kiikolojia kinacholinda haki za kijamii, kukuza ajira, kulinda bayoanuwai, na kuboresha afya ya udongo na mazingira.

Waandishi wa habari Waandamizi kutoka nchi kadhaa Afrika ikiwepo, Tanzania,Kenya,Uganda,Malawi,Zambia,Togo,Tunisia,Zimbabwe,Ghana,Burkinafaso na wenyeji ,Ethiopia wanashiriki mafunzo hayo.

Na Serengeti Media Centre - Mugumu.CPA. Catherine Ruge leo Julai 22, 2025 amerejesha fomu ya kuwania nafasi ya Ubunge Ji...
22/07/2025

Na Serengeti Media Centre - Mugumu.

CPA. Catherine Ruge leo Julai 22, 2025 amerejesha fomu ya kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Serengeti kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA).

Ruge amesema akipata ridhaa atawatumikia wananchi kwa weledi mkubwa huku akiipambania nafasi za vijana na wanawake wa Serengeti katika kuleta maendeleo.

Zaidi Tazama Youtube Yetu

MRADI WA MAJI MUSATI WAPATA TIBA, WANANCHI WAIPONGEZA RUWASA NA SERENGETI MEDIANa Serengeti Media Centre – MusatiHatimay...
22/07/2025

MRADI WA MAJI MUSATI WAPATA TIBA, WANANCHI WAIPONGEZA RUWASA NA SERENGETI MEDIA

Na Serengeti Media Centre – Musati

Hatimaye mradi wa maji ya mtiririko katika chanzo cha Mto Musati kilichopo Kijiji cha Musati Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara kinatarajiwa kufanyiwa marekebisho makubwa baada ya kuharibiwa na mvua za Elinino mwaka 2023 hali iliyowapelekea wakazi wa Kijiji hicho kutumia maji yasiyo safi na salama.

Marekebisho hayo yanafuata baada ya Mtandao wa Serengeti Media Centre na Antomatv Online kupaza sauti kuhusu kuharibika kwa chanzo hicho hadi kupelekea kupatikana kwa mkandarasi kutoka Kampuni ya Kojas Builders ya Jijini Mwanza ambaye ameshasaini mkataba wa miezi sita.

Akiongea na wakazi wa Kijiji hicho Mhandisi Deus Mchele Meneja wa Wakala wa Maji Vijijiji (RUWASA) amesema gharama za mradi hadi huo hadi kukamilika kwakwe ni Sh 284 Mil. kazi ndogo ngogo 21 zitafanywa ikiwemo ujenzi wa barabara kuelekea eneo la chanzo.

“Tulipofanya tathimini ya uharibifu tulitegemea kufanya kazi kwa kutumia ‘Force Acount’ mvua ilipozidi kuharibu tulilazimika kumtafuta mkandarasi mwenye uwezo mkubwa wa vifaa na uchumi” amesema Mhandisi Deus na kuongeza kuwa,

“Tumekuja kumuonesha mkandarasi eneo la mradi ilia apate ramani kamili na namna nzuri ya kuujenga mradi, kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa tumemsisitizia aweze kufanya kazi kwa haraka ndani ya miezi miwili ili wananchi wapate huduma ya maji k**a awali” amesema Mhandisi Deus.

Mhandisi Nyerere Lucas kutoka Kojas Builders amesema “nimeona eneo husika na kile kinachotakiwa, timu yetu imejipanga vyema baada ya wiki mbili tutaleta mitambo na tutajitahidi kuifanya kazi kwa mapema ili ndani ya hiyo miezi miwili tukabidhi” amesema Mhandisi Nyerere.

Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kebanchabancha Chacha Matikho amesema “naishukuru Serengeti Media na RUWASA kwa kuwa nasi bega kwa bega, tumepambana nao toka mwanzo wa tatizo, matumaini yangu kwenu wananchi pindi mradi utakapokamilika tutachangia huduma ili uweze kudumu”.

Matikho amesema amepigania miradi mbalimbali katani hapo ikiwemo mradi wa maji wa Kebanchabancha wa Kisima kirefu cha Kebagusuhi uliotekelezwa na RUWASA kwa zaidi ya Sh 200 Mil.

Mwita Kebaki Mkazi wa Kijiji cha Musati amesema “mvua ndio imetuletea adha kwa kipindi cha miaka miwili sasa, nawashukuru Serengeti Media kwa kutusemea sambamba na RUWASA kwa kututafutia suluhisho”.

Endelea Kuwa Nasi

Tanapa yachukua hatua kwa madereva wanaoruhusu wageni kushuka hifadhini.
21/07/2025

Tanapa yachukua hatua kwa madereva wanaoruhusu wageni kushuka hifadhini.

WETCU 2018 LTD  WAJIPANGA KIMKAKATI MAONESHO YA NANE NANESerengeti Media Centre-Tabora.Chama Kikuu cha Ushirika cha WETC...
21/07/2025

WETCU 2018 LTD WAJIPANGA KIMKAKATI MAONESHO YA NANE NANE

Serengeti Media Centre-Tabora.

Chama Kikuu cha Ushirika cha WETCU 2018 LTD chenye Makao Makuu yake Mkoani Tabora,kwa kushirikiana na Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania(TCDC)na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC) kimejipanga kuonesha bidhaa mbalimbali wakati wa maonesho ya Nane nane Dodoma.

Meneja Mkuu wa WETCU 2018 Samwel Jokeya ameiambia Serengeti Media Media na Antoma Tv Online kuwa,wanawaalika wananchi wa Dodoma na Mikoa mingine kupata na kuona bidhaa mbalimbali k**a unga wa Sembe wanaozalisha wao wenyewe.

“Tutashiriki maonesho ya Nane nane katika Kijiji cha Ushirika,viwanja vya Nzuguni Dodoma kwa kuwa tumejipanga kimkakati kuwapatia bidhaa tunazozalisha k**a unga wa sembe,pia kuona tumbaku,mbolea,viuatilifu,vifungashio vya tumbaku,vifaa kinga na huduma za elimu ya ugani”amesema.

Amesema,wanatoa fursa mbalimbali k**a utafutaji wa masoko ya tumbaku,kuratibu na upatikanaji wa pembejeo za kilimo,huduma za ugani kwa wanachama na makundi mbalimbali ya kijamii.

Naye Neema Changamike toka chama hicho amesema,mbali ya huduma za ugani pia wanatoa huduma za Tehama,ikiwemo kuwatafutia wakulima masoko ya alizeti,”tunawakaribisha wanaushirika,wote,wadau na wananchi kwa ajili ya kupata huduma bora za kiuchumi”amesema.

Endelea Kuwa Nasi.

Address


Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Serengeti Media Centre posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Serengeti Media Centre:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share