Hasanaatu TV

Hasanaatu TV Page hii inahusu kusambaza Yalio mema na Kukumbushana kwa yanayo tuzunguka katika jamii

𝗧𝗔𝗡𝗭𝗜𝗔إنا لله وإنا إليه راجعون اللهم Sheikh  ́Abdul-ʿAzīz ibn  ́Abdullah Āl al-Shaykh, M***i Mkuu wa Ufalme wa Saudi Ara...
23/09/2025

𝗧𝗔𝗡𝗭𝗜𝗔

إنا لله وإنا إليه راجعون اللهم

Sheikh ́Abdul-ʿAzīz ibn ́Abdullah Āl al-Shaykh, M***i Mkuu wa Ufalme wa Saudi Arabia, amefariki dunia leo 23/09/2025.

Swala ya jeneza (maiti) itasaliwa leo katika Msikiti wa Imam Turki bin Abdullah mjini Riyadh baada ya swala ya ́Asr.

Ewe Mwenyezi Mungu, msamehe Sheikh Abdul-Aziz, inua daraja yake miongoni mwa walioongoka, na mpe urithi mzuri katika kizazi chake, utusamehe sisi na yeye, Ewe Mola wa walimwengu wote, mpanulie kaburi lake na ulijaze nuru. Allaahumma Aamiyn.

Hakika sisi Sote ni wa Mwenyezi Mungu na Kwake ndiyo Marejeo.

Allah atujaalie mwisho mwema

Ungana nasi kwa taarifa sahihi.
__________




بِسْمِ اللهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ *KUPATWA KWA JUA NA MWEZI* *Hukmu, Sayansi na Mafunzo.* (*The Eclipse of the Sun and...
07/09/2025

بِسْمِ اللهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ

*KUPATWA KWA JUA NA MWEZI*

*Hukmu, Sayansi na Mafunzo.*
(*The Eclipse of the Sun and Moon: Rulings, Science & Reflections*)
*الكُسوف والخُسوف: الأحكام والعِلم والعِبَر*
---

*1. MAAANA YA KUPATWA* :

- *كُسُوف الشمس*: Ni Hali ambapo mwezi unazuia mwanga wa jua kwa muda.
- *خُسُوف القمر*:
Ni Hali ambapo mwezi hauonekani kwa sababu ya kuingia kwenye kivuli cha dunia.
---

*2. SABABU YA KISAYANSI*

- Kupatwa kwa jua (Solar Eclipse) hutokea mwezi unapopita kati ya dunia na jua.
- Kupatwa kwa mwezi (Lunar Eclipse) hutokea dunia inapopita kati ya jua na mwezi.

Haya yote ni mzunguko wa kiasili uliowekwa na Allah, si tukio la kishetani wala la bahati mbaya.
---

*3. DALILI ZA KISHARIA*

*QUR’ĀN:*

وَمَا نُرْسِلُ بِالْآيَاتِ إِلَّا تَخْوِيفًا
*“Wala hatutumi Ishara isipokuwa kwa ajili ya kuwatia watu khofu.”*
(Sūrat Al-Isrā: 59)

*وَمِنْ آيَاتِهِ ٱلَّيْلُ وَٱلنَّهَارُ وَٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ ۚ لَا تَسْجُدُوا۟ لِلشَّمْسِ وَلَا لِلْقَمَرِ وَٱسْجُدُوا۟ لِلَّهِ ٱلَّذِى خَلَقَهُنَّ إِن كُنتُمْ إِيَّاهُ تَعْبُدُونَ*
(فصلت: 37)
*Maana:* *Na miongoni mwa ishara zake ni usiku, mchana, jua na mwezi. Msisujudie jua wala mwezi bali msujudieni Allah aliyeviumba k**a kweli mnamuabudu.*
(Surah Fuswilat)

*HADĪTH SAHIHI:*

إِنَّ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ آيَتَانِ مِنْ آيَاتِ اللَّهِ، لَا يَنْخَسِفَانِ لِمَوْتِ أَحَدٍ وَلَا لِحَيَاتِهِ، فَإِذَا رَأَيْتُمُوهُمَا فَصَلُّوا وَادْعُوا حَتَّى يَنْجَلِيَ مَا بِكُمْ. مسلم

*“Hakika jua na mwezi ni miongoni mwa alama za Allah. Havipatwi kwa sababu ya kufa kwa mtu au kuzaliwa kwake. Basi mnapoviona vikipatwa, salini, ombeni, hadi yakae sawa.”*
(Imam Muslim)
---

*4. HUKUMU YA SWALA YA KUPATWA*:

- Ni *Sunnah Mu’akkadah*.
- Haiswaliwi kwa adhana wala iqaamah.
- Inaswaliwa kwa jamaa au mtu mmoja.
- Raka’a mbili tu, kila raka’a ina kusoma mara mbili na rukuu mbili.
- Muda wake huendelea hadi kupatwa kumalizike.

*NAMNA YA KUSWALI*:

- Raka’a mbili
- Kila raka’a ina rukuu mbili (rukuu ya kwanza ndefu, ya pili fupi)
- Kila raka’a ina kusoma mara mbili (baada ya qiyām).

*5. TOFAUTI KATI YA SWALA YA KUSUUF NA KHUSUUF* :

- Kusūf (kupatwa kwa jua) huswaliwa mchana kwa *sauti ya siri* (sirriyah), na kuna *khutba* baada ya swala.
- Khusūf (kupatwa kwa mwezi) huswaliwa usiku kwa *sauti ya juu* (jahr), na *hakuna khutba*.
---

*6. NANI HASWALI, NA AFANYE NINI?*:

- Mwanamke aliye hedhi au nifās: Hataswali, lakini atajishughulisha na *dhikr, istighfār, na dua*.
- Wagonjwa au walio safarini: Waswali kwa hali waliyo nayo– kwa kukaa au kulala.
- Watoto: Inafaa kuwahusisha kwa kujifunza na mazoezi ya dini.
---

*7. MAMBO YA KUFANYA WAKATI WA KUPATWA*:

Mtume صلى الله عليه وسلم alisema:

فَافْزَعُوا إِلَى الصَّلَاةِ
*"Kimbilieni swala!"*
(Sahih Muslim)

Mambo ya kuamrishwa:

- Swala
- Dua na istighfār
- Kutoa sadaka
- Kuhimiza toba na kurudi kwa Allah
---

*8. MAFUNZO TUNAYO PATA*

- Kupatwa ni onyo na ukumbusho wa *siku ya Qiyāmah*.
- Hufundisha kuwa uweza wote ni wa *Allāh سبحانه وتعالى*.
- Sayansi haipingani na dini, bali huthibitisha *ukuu wa Muumba*.
- Muumini wa kweli hubadilika na kuongeza ibada kwa kuona aya k**a hizi.
---

*9. HUKUMU KWA WALIO DHARURA*

- Mwanamke aliye kwenye udhuru halazimiki kuswali, lakini *asikose dua na kumkumbuka Allah*.
- Ikiwa kupatwa kutatokea na hawezi kushiriki kwa jamaa, *anaruhusiwa kuswali peke yake*.
- Aliyeshindwa hata kuswali, anaweza *kumuomba Allah kwa moyo, machozi, na dua.*
---

*10. HITIMISHO*

Kupatwa kwa jua au mwezi ni aya na alama kubwa ya uwepo wa Allah. Tusichukulie kwa mzaha wala k**a tukio la kawaida. Bali tuswali, tuombe rehema ya Allah, turejee kwa toba, na tusahihishe hali zetu kwa ajili ya Akhera.

Ameandaa
📚🖋️ *Sheikh*
*Abdurrahmani M***a*
(Allah amlipe kheri)
_______




30/08/2025



Hakika dini yetu tukufu ya Kiislamu imehimiza sana umuhimu wa kushik**ana na elimu ya Dini, na kufanya juhudi ya kufundishana na kukumbushana kheri miongoni mwa Waislamu.

📌 UMUHIMU WA YA DINI:
Elimu ya Dini ni nuru inayomuongoza mtu kuelekea kumpendeza Allah, kujiepusha na haramu, na kuishi maisha yenye nidhamu, adabu, na mafanikio ya dunia na Akhera.

*🕌 Muongozo wa Wanachuoni:*
Imam Ahmad bin Hanbal (رحمه الله) amesema:
*"الناس محتاجون إلى العلم أكثر من حاجتهم إلى الطعام والشراب"*
_“Watu wanahitajia elimu zaidi kuliko wanavyohitajia chakula na kinywaji.”_

*📖 Hadithi ya Mtume ﷺ:*
Mtume صلى الله عليه وسلم amesema:
*"مَنْ سَلَكَ طَرِيقًا يَلْتَمِسُ فِيهِ عِلْمًا، سَهَّلَ اللَّهُ لَهُ بِهِ طَرِيقًا إِلَى الْجَنَّةِ"*
_“Yeyote atakayechukua njia ya kutafuta elimu, basi Allah atamrahisishia kwa hiyo njia njia ya kuelekea Peponi.”_
(Hadithi – Imepokewa na Muslim)

*📝 Hitimisho:*
Tuchangamkie fursa ya kusambaza mawaidha, kusikiliza, na kufundisha Dini kwa njia yoyote halali. Ni katika njia bora kabisa ya kutafuta radhi za Allah na kusaidia jamii.

*🔁 Share kwa wengine ili faida iwafikie pia.*
* *

Address

6 Valk Street
Kinross
2270

Telephone

+27724656380

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hasanaatu TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hasanaatu TV:

Share

Category