Hasanaatu TV

Hasanaatu TV Page hii inahusu kusambaza Yalio mema na Kukumbushana kwa yanayo tuzunguka katika jamii

𝗧𝗔𝗡𝗭𝗜𝗔إنا لله وإنا إليه راجعون اللهم Sheikh  ́Abdul-ʿAzīz ibn  ́Abdullah Āl al-Shaykh, M***i Mkuu wa Ufalme wa Saudi Ara...
23/09/2025

𝗧𝗔𝗡𝗭𝗜𝗔

إنا لله وإنا إليه راجعون اللهم

Sheikh ́Abdul-ʿAzīz ibn ́Abdullah Āl al-Shaykh, M***i Mkuu wa Ufalme wa Saudi Arabia, amefariki dunia leo 23/09/2025.

Swala ya jeneza (maiti) itasaliwa leo katika Msikiti wa Imam Turki bin Abdullah mjini Riyadh baada ya swala ya ́Asr.

Ewe Mwenyezi Mungu, msamehe Sheikh Abdul-Aziz, inua daraja yake miongoni mwa walioongoka, na mpe urithi mzuri katika kizazi chake, utusamehe sisi na yeye, Ewe Mola wa walimwengu wote, mpanulie kaburi lake na ulijaze nuru. Allaahumma Aamiyn.

Hakika sisi Sote ni wa Mwenyezi Mungu na Kwake ndiyo Marejeo.

Allah atujaalie mwisho mwema

Ungana nasi kwa taarifa sahihi.
__________




بِسْمِ اللهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ *KUPATWA KWA JUA NA MWEZI* *Hukmu, Sayansi na Mafunzo.* (*The Eclipse of the Sun and...
07/09/2025

بِسْمِ اللهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ

*KUPATWA KWA JUA NA MWEZI*

*Hukmu, Sayansi na Mafunzo.*
(*The Eclipse of the Sun and Moon: Rulings, Science & Reflections*)
*الكُسوف والخُسوف: الأحكام والعِلم والعِبَر*
---

*1. MAAANA YA KUPATWA* :

- *كُسُوف الشمس*: Ni Hali ambapo mwezi unazuia mwanga wa jua kwa muda.
- *خُسُوف القمر*:
Ni Hali ambapo mwezi hauonekani kwa sababu ya kuingia kwenye kivuli cha dunia.
---

*2. SABABU YA KISAYANSI*

- Kupatwa kwa jua (Solar Eclipse) hutokea mwezi unapopita kati ya dunia na jua.
- Kupatwa kwa mwezi (Lunar Eclipse) hutokea dunia inapopita kati ya jua na mwezi.

Haya yote ni mzunguko wa kiasili uliowekwa na Allah, si tukio la kishetani wala la bahati mbaya.
---

*3. DALILI ZA KISHARIA*

*QUR’ĀN:*

وَمَا نُرْسِلُ بِالْآيَاتِ إِلَّا تَخْوِيفًا
*“Wala hatutumi Ishara isipokuwa kwa ajili ya kuwatia watu khofu.”*
(Sūrat Al-Isrā: 59)

*وَمِنْ آيَاتِهِ ٱلَّيْلُ وَٱلنَّهَارُ وَٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ ۚ لَا تَسْجُدُوا۟ لِلشَّمْسِ وَلَا لِلْقَمَرِ وَٱسْجُدُوا۟ لِلَّهِ ٱلَّذِى خَلَقَهُنَّ إِن كُنتُمْ إِيَّاهُ تَعْبُدُونَ*
(فصلت: 37)
*Maana:* *Na miongoni mwa ishara zake ni usiku, mchana, jua na mwezi. Msisujudie jua wala mwezi bali msujudieni Allah aliyeviumba k**a kweli mnamuabudu.*
(Surah Fuswilat)

*HADĪTH SAHIHI:*

إِنَّ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ آيَتَانِ مِنْ آيَاتِ اللَّهِ، لَا يَنْخَسِفَانِ لِمَوْتِ أَحَدٍ وَلَا لِحَيَاتِهِ، فَإِذَا رَأَيْتُمُوهُمَا فَصَلُّوا وَادْعُوا حَتَّى يَنْجَلِيَ مَا بِكُمْ. مسلم

*“Hakika jua na mwezi ni miongoni mwa alama za Allah. Havipatwi kwa sababu ya kufa kwa mtu au kuzaliwa kwake. Basi mnapoviona vikipatwa, salini, ombeni, hadi yakae sawa.”*
(Imam Muslim)
---

*4. HUKUMU YA SWALA YA KUPATWA*:

- Ni *Sunnah Mu’akkadah*.
- Haiswaliwi kwa adhana wala iqaamah.
- Inaswaliwa kwa jamaa au mtu mmoja.
- Raka’a mbili tu, kila raka’a ina kusoma mara mbili na rukuu mbili.
- Muda wake huendelea hadi kupatwa kumalizike.

*NAMNA YA KUSWALI*:

- Raka’a mbili
- Kila raka’a ina rukuu mbili (rukuu ya kwanza ndefu, ya pili fupi)
- Kila raka’a ina kusoma mara mbili (baada ya qiyām).

*5. TOFAUTI KATI YA SWALA YA KUSUUF NA KHUSUUF* :

- Kusūf (kupatwa kwa jua) huswaliwa mchana kwa *sauti ya siri* (sirriyah), na kuna *khutba* baada ya swala.
- Khusūf (kupatwa kwa mwezi) huswaliwa usiku kwa *sauti ya juu* (jahr), na *hakuna khutba*.
---

*6. NANI HASWALI, NA AFANYE NINI?*:

- Mwanamke aliye hedhi au nifās: Hataswali, lakini atajishughulisha na *dhikr, istighfār, na dua*.
- Wagonjwa au walio safarini: Waswali kwa hali waliyo nayo– kwa kukaa au kulala.
- Watoto: Inafaa kuwahusisha kwa kujifunza na mazoezi ya dini.
---

*7. MAMBO YA KUFANYA WAKATI WA KUPATWA*:

Mtume صلى الله عليه وسلم alisema:

فَافْزَعُوا إِلَى الصَّلَاةِ
*"Kimbilieni swala!"*
(Sahih Muslim)

Mambo ya kuamrishwa:

- Swala
- Dua na istighfār
- Kutoa sadaka
- Kuhimiza toba na kurudi kwa Allah
---

*8. MAFUNZO TUNAYO PATA*

- Kupatwa ni onyo na ukumbusho wa *siku ya Qiyāmah*.
- Hufundisha kuwa uweza wote ni wa *Allāh سبحانه وتعالى*.
- Sayansi haipingani na dini, bali huthibitisha *ukuu wa Muumba*.
- Muumini wa kweli hubadilika na kuongeza ibada kwa kuona aya k**a hizi.
---

*9. HUKUMU KWA WALIO DHARURA*

- Mwanamke aliye kwenye udhuru halazimiki kuswali, lakini *asikose dua na kumkumbuka Allah*.
- Ikiwa kupatwa kutatokea na hawezi kushiriki kwa jamaa, *anaruhusiwa kuswali peke yake*.
- Aliyeshindwa hata kuswali, anaweza *kumuomba Allah kwa moyo, machozi, na dua.*
---

*10. HITIMISHO*

Kupatwa kwa jua au mwezi ni aya na alama kubwa ya uwepo wa Allah. Tusichukulie kwa mzaha wala k**a tukio la kawaida. Bali tuswali, tuombe rehema ya Allah, turejee kwa toba, na tusahihishe hali zetu kwa ajili ya Akhera.

Ameandaa
📚🖋️ *Sheikh*
*Abdurrahmani M***a*
(Allah amlipe kheri)
_______




30/08/2025



Hakika dini yetu tukufu ya Kiislamu imehimiza sana umuhimu wa kushik**ana na elimu ya Dini, na kufanya juhudi ya kufundishana na kukumbushana kheri miongoni mwa Waislamu.

📌 UMUHIMU WA YA DINI:
Elimu ya Dini ni nuru inayomuongoza mtu kuelekea kumpendeza Allah, kujiepusha na haramu, na kuishi maisha yenye nidhamu, adabu, na mafanikio ya dunia na Akhera.

*🕌 Muongozo wa Wanachuoni:*
Imam Ahmad bin Hanbal (رحمه الله) amesema:
*"الناس محتاجون إلى العلم أكثر من حاجتهم إلى الطعام والشراب"*
_“Watu wanahitajia elimu zaidi kuliko wanavyohitajia chakula na kinywaji.”_

*📖 Hadithi ya Mtume ﷺ:*
Mtume صلى الله عليه وسلم amesema:
*"مَنْ سَلَكَ طَرِيقًا يَلْتَمِسُ فِيهِ عِلْمًا، سَهَّلَ اللَّهُ لَهُ بِهِ طَرِيقًا إِلَى الْجَنَّةِ"*
_“Yeyote atakayechukua njia ya kutafuta elimu, basi Allah atamrahisishia kwa hiyo njia njia ya kuelekea Peponi.”_
(Hadithi – Imepokewa na Muslim)

*📝 Hitimisho:*
Tuchangamkie fursa ya kusambaza mawaidha, kusikiliza, na kufundisha Dini kwa njia yoyote halali. Ni katika njia bora kabisa ya kutafuta radhi za Allah na kusaidia jamii.

*🔁 Share kwa wengine ili faida iwafikie pia.*
* *

𝗠𝗔𝗛𝗠𝗢𝗨𝗗 𝗠𝗔𝗬𝗘𝗟𝗘(FISTON  MAYELE)Mshambuliaji wa zamani wa Yanga {Raia wa DRC Congo} ambae kwa sasa anakipiga Kwenye klabu ...
16/07/2025

𝗠𝗔𝗛𝗠𝗢𝗨𝗗 𝗠𝗔𝗬𝗘𝗟𝗘
(FISTON MAYELE)
Mshambuliaji wa zamani wa Yanga {Raia wa DRC Congo} ambae kwa sasa anakipiga Kwenye klabu ya Pyramids FC ya Misri, Fiston Mayele amebadilisha dini kutoka kuwa Mkristo na sasa ni Muislamu

Ripoti zinaeleza kuwa Mayele amebadilisha dini miezi sita iliyopita na hata kipindi cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan alikuwa akijumuika na wenzake waliofunga

Uamuzi wa Mayele kubadili dini ulisababishwa na wachezaji wenzake wa Pyramids FC, haswa Ramadan Sobhi na Karim Hafez, na inaripotiwa kuwa maamuzi hayo aliyafikia kipindi cha mwezi wa Ramadhani.

Baada ya kubadilisha dini kwa sasa Mayele hatambuliki k**a Fiston Mayele bali amechagua jina la Mahmoud na hivyo anaitwa Mahmoud Mayele.

Anasema Allaah (ﷻ) Mtukufu:

{ إِذَا جَآءَ نَصۡرُ ٱللَّهِ وَٱلۡفَتۡحُ }

"Itakapo kuja nusura ya Mwenyezi Mungu na ushindi,"

{ وَرَأَيۡتَ ٱلنَّاسَ يَدۡخُلُونَ فِي دِينِ ٱللَّهِ أَفۡوَاجٗا }

"Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Mwenyezi Mungu kwa makundi,"

{ فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَٱسۡتَغۡفِرۡهُۚ إِنَّهُۥ كَانَ تَوَّابَۢا }

"Zitakase sifa za Mola wako Mlezi, na umwombe msamaha; hakika Yeye ndiye anaye pokea toba".

[Surat An-Nasr: 1-3]

Ungana nasi kwa habari sahihi
na zenye uhakika

Follow Us



Fahamu yalio mema

16/07/2025

UPDATES

INNA LILLAHI WA INNA
ILAIHI RAJIUN

MSIBA MKUBWA !!

AMEFARIKI {15-07-2025}
HAFIDH MKUBWA WA QUR'AN TUKUFU NA KIJANA ILIYE ITUMIKIA QUR'AN NA KUIFANYIA KAZI HAFIZ
SOW
KUTOKA NCHI YA COTÉ D'IVOIRE, PIA ALIKUA MSHINDI WA 1 KWENYE MASHINDANO MAKUBWA YA QURANI TUKUFU MWAKA JANA { 2024} YALIO ANDALIWA NA Al-Hikma Qur'an Competition CHINI YA USIMAMIZI WA SHEIKH NURDIN Kishki Jijini Dar es salaam nchini Tanzania

Hakika kifo ni fumbo, tuishi katika misingi anayo iridhia na kuipenda Allah, hakika kijana ameondoka akiwa na umri mdogo kwanza ndo Ana umri wa myaka 15 na sababu ya kifo chake ni maradhi ya muda mfupi, tunataraji kheri na mafikio mazuri kutokana na utukufu wa Qur'an aliyo ibeba katika kifua chake, hakika alikua kijana mwenye mfano wa kuigwa hasa katika ulimwengu wa Qur'an, kwani alishindana Mashindano mengi ya Qur'an ndani na nje ya nchi yake na alikua akiibuka mshindi Alhamdulillah...

ALLAH Amrehemu na amsamehe alipo teleza na Allah ajaalie Quran iwe ni utetezi wake Aamiin

Ungana nasi kwa Habari
Sahihi na za uhakika

Subscribe & follow Us




To Allah we belong and to him we all shall return.
We are saddened to announce the death of our Dear brother, Qari Ibrahim Sow from Ivory Coast,

He was the winner of the Tanzania International Quranic competition just last year 2024.
He is well known for his powerful recitation and participation in many international and local Quranic competitions.

May Allah Overlooked his mistake and grant him the highest part of Jannah.

Foe more
Subscribe & follow Us

UPDATESHABARI NJEMA KUTOKA JIJINI BUJUMBURA NCHINI BURUNDIHATUA NZURI KUTOKA KWA SHEIKH  .NA UONGOZI WA  Baada ya kufany...
13/07/2025

UPDATES

HABARI NJEMA KUTOKA JIJINI BUJUMBURA NCHINI BURUNDI

HATUA NZURI KUTOKA KWA SHEIKH .
NA UONGOZI WA

Baada ya kufanya Ziara yaki Da'awah nchini Burundi kwa siku kadhaa, Leo Alihitimisha Ziara yake kwa tukio kubwa na Lakihistoria nchini humo, na hayo yamefanyika akiwa sambamba na M***i wa Burundi (Pichani na Sheikh kishki) Tukio Hilo ilikua ni kufungisha ndoa ya kihistoria ya watu mia moja (100) kupitia taasisi yake ya .

Katika Siku ya leo Jumapili ya tarehe 13/07/2025.
Ndani ya Jiji la

Allah Amlipe Sheikh kila la kheri
Napia kila aliye shiriki katika
Kukamilika kwa Jambo Hilo
Allah amlipe kheri kwa nia njema

Jiunge nasi kwa Habari za
Kheri na zenye uhakika





Fahamu yalio mema.

25/06/2025

Alhamdulillah Tumeingia katika mwaka mpya wa kiislam_Muharram 1447 H

EID MUBARAKA kwa Waislamu wote Duniani   Ungana nasi kwa mengi zaidi
05/06/2025

EID MUBARAKA
kwa Waislamu
wote Duniani




Ungana nasi kwa mengi zaidi

SIKU 10 ZA MWANZO KATIKA DHUL HIJJAH _______________________{} "KUMI LA MWANZO LA DHUL-HIJJAH" 👇Katika siku hizi kumi, k...
28/05/2025

SIKU 10 ZA MWANZO
KATIKA DHUL HIJJAH
_______________________

{} "KUMI LA MWANZO LA DHUL-HIJJAH" 👇

Katika siku hizi kumi, kuna: 👇🏾

1- Siku ambayo kufunga ni makubaliano ya wote, nayo ni siku ya Arafah.

2- Siku ambayo haifungwi kwa makubaliano ya wote, nayo ni siku ya Eid (Yawm an-Nahr).

3- Na kuna siku ambazo kuna tofauti ya maoni, nazo ni zile siku nane za mwanzo.

Kauli iliyo na uzito zaidi ni kuwa inapendelewa kufunga siku yoyote inayowezekana kati ya hizo, kwa kuwa ni miongoni mwa matendo mema.

Mtume ﷺ amesema:

> "Hakuna siku ambazo matendo mema yanapendwa zaidi kwa Mwenyezi Mungu kuliko katika siku hizi (kumi)."

Wakasema: Hata jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu?

Akasema ﷺ:

> "Hata jihadi, isipokuwa mtu aliyetoka na nafsi yake na mali yake, kisha asirudi na chochote (yaani, akapoteza vyote kwa ajili ya Allah)."
(Riwaya ya Bukhari)

Kazi bora kabisa ya ibada katika siku hizi, ambayo wanazuoni wote wamekubaliana kuwa ni sunna, ni kutamka dhikr kwa sauti kubwa, yaani kumkumbuka Allah kwa sauti.

Allah Ta'ala amesema:

> (“…na walitaje jina la Allah katika siku maalumu…”) — Al-Hajj: 28

Ibn Abbas (r.a) amesema:

> "Siku maalumu ni siku kumi za Dhul-Hijjah."

Na Ibn Umar na Abu Hurairah (r.a) walikuwa wakitoka kwenda sokoni katika siku hizi na wanatoa takbira kwa sauti, na watu wengine walikuwa wakitakbiri kwa kusikia takbira zao.

(Riwaya ya Bukhari kwa njia ya ta’liq lakini ni yenye hukumu ya kuaminika)

Miongoni mwa takbira sahihi zaidi ni hizi mbili:

(1) . Allahu Akbar, Allahu Akbar, Allahu Akbar, la ilaha illa Allah, Allahu Akbar, Allahu Akbar wa lillahil-hamd.

(2) . Allahu Akbar, Allahu Akbar, Allahu Akbar kabīrā, Allahu a‘lā wa ajall, Allahu Akbar wa lillāhil-hamd.

Ungana nasi kwa elimu na mengi mazuri na sahihi kabisa Kisha Share kwa wengine


Fahamu yaliyo mema

UKUMBUSHO KUHUSU HIJJAH
30/04/2025

UKUMBUSHO KUHUSU HIJJAH


𝗦𝗛𝗘𝗞𝗛 𝗦𝗪𝗔𝗟𝗘𝗛 𝗔𝗟 𝗙𝗔𝗪𝗭𝗔𝗔𝗡 Shekh Abdul Aziz Ibn Baz (Allah Amrehem), alipoulizwa ni nani tumuulize baada yako, akajibu: "Al...
26/04/2025

𝗦𝗛𝗘𝗞𝗛 𝗦𝗪𝗔𝗟𝗘𝗛 𝗔𝗟 𝗙𝗔𝗪𝗭𝗔𝗔𝗡

Shekh Abdul Aziz Ibn Baz (Allah Amrehem), alipoulizwa ni nani tumuulize baada yako, akajibu: "Al-Fawzan"..

Shekh Muhammad Ibn Uthaymiyn (Allah Amrehem) alipoulizwa ni nani tumuulize baada yako, Akajibu: "Muulize Al-Fawzan."
Aliwahi kusema: Moyo hutulizwa na fatwa za Sheikh (maana yake Al-Fawzan)...

Huyu ndiye Sheikhul Islam (Shekh wa Uislamu) katika zama hizi na ni katika wenye elimu kubwa Alhamdulillah ...

Allaah Amlinde Sheikh wetu mbora, mwanachuoni na Doktor Muhammad Swaleh bin Fawzan Al-Fawzan, Allah Amzidishie umri na Aziongoze hatua zake, yeye na masheikh wote watetezi wa Sunnah . Aamiyn🤲

𝗙𝗢𝗟𝗟𝗢𝗪 𝗙𝗕 𝗣𝗔𝗚𝗘

Eid Mubaaraka to all MuslimsAllah atupokelee matendo yetu
29/03/2025

Eid Mubaaraka to all Muslims
Allah atupokelee matendo yetu



Address

6 Valk Street
Kinross
2270

Telephone

+27724656380

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hasanaatu TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hasanaatu TV:

Share

Category