Sports campaign tz

Sports campaign tz Sports and Entertainment

AHMED ALLY AWATULIZA MASHABIKI KUHUSU MPANZU: "YUKO WAPI?"Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba SC, Ahmed Al...
04/08/2025

AHMED ALLY AWATULIZA MASHABIKI KUHUSU MPANZU: "YUKO WAPI?"

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba SC, Ahmed Ally, ameibuka na kuwashangaa baadhi ya wachambuzi na wanahabari wanaoeneza taarifa zisizo na uhakika kuhusu mchezaji wao Elie Mpanzu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ahmed amesema amebaki kushangazwa na kauli zinazokinzana kutoka kwa watu wale wale waliodai awali kuwa Mpanzu hayuko Misri, lakini sasa wamesema ameonekana nchini humo.

“Kinachonishangaza ni kwamba watu waliokuwa wakisema Mpanzu hayupo Misri, ni hao hao leo wanasema amefika Misri,” ameandika Ahmed, huku akiwataka wenye taarifa za uhakika wamsaidie kwa kumwelekeza mchezaji huyo kwani wao hawajamuona.

Ameongeza kuwa si vema kueneza taharuki kwa mashabiki, bali watu waendelee kuwa na amani huku wakisubiri taarifa rasmi kutoka kwa klabu.

Katika siku za karibuni, kumekuwepo na ongezeko la taarifa na tetesi mbalimbali kuhusu usajili wa wachezaji baina ya vigogo wa soka nchini — Simba SC na Yanga SC — hali inayowaweka mashabiki wa pande zote za Kariakoo katika hali ya taharuki.

SWALI KWA MASHABIKI:
JE, UNADHANI ELIE MPANZU ATABAKIA SIMBA AU ATAELEKEA YANGA? NA JE, NAFASI YAKE YA KUNG'AA NI KUBWA ZAIDI AKIWA SIMBA AU YANGA?

TUJADILIANE.

TOTO AFRICANS YAKWAMA KUINUA ILIPOLALA.Timu ya Toto Africans imeshindwa kupata mafanikio katika Soka,  licha ya kuwa na ...
04/08/2025

TOTO AFRICANS YAKWAMA KUINUA ILIPOLALA.

Timu ya Toto Africans imeshindwa kupata mafanikio katika Soka, licha ya kuwa na jengo katikati ya jiji la Mwanza.

Zipo sababu nyingi na zinahusisha mambo ya kiutawala, kiuchumi, na kimkakati. Hizi hapa ni sababu kuu:

1. Matumizi Mabaya au Yasiyo na Mpango wa Mali (Jengo)

Licha ya kuwa na jengo katika eneo la kimkakati (katikati ya jiji), taarifa zinaonesha kuwa halikuendelezwa ipasavyo k**a kitega uchumi. Mapato yaliyotokana na jengo hilo hayakuwekezwa moja kwa moja kwenye timu au maendeleo ya michezo.

2. Uongozi Dhaifu na Mvurugano wa Ndani

Toto Africans kwa muda mrefu imekuwa na migogoro ya kiuongozi – mara nyingi viongozi walikosa umoja, mipango ya muda mrefu, na uwazi wa kifedha. Hii ilisababisha kushindwa kutumia rasilimali walizonazo kwa ufanisi.

3. Ukosefu wa Mpango wa Kibiashara

Licha ya kuwa katika jiji lenye fursa nyingi za kibiashara (Mwanza), Toto Africans haikuweka mfumo wa kibiashara endelevu k**a kuuza bidhaa za klabu, mikataba ya wadhamini, au huduma nyingine za kuepuka utegemezi wa wafadhili au matoleo ya hisani.

4. Kutokuwepo kwa Miundombinu Bora ya Michezo

Pamoja na kuwa na jengo, timu haikuwa na kambi ya kudumu au uwanja wa mazoezi wa kisasa. Hii iliathiri maendeleo ya kiufundi ya wachezaji na uwezo wa kuvutia vipaji vipya.

5. Kukosekana kwa Mkakati wa Kuendeleza Vipaji

Tofauti na timu k**a Azam au Yanga zenye akademi za kukuza vijana, Toto Africans haikuwekeza kikamilifu katika vipaji vya ndani vya Mwanza au mikoa jirani. Hii ilisababisha timu kutegemea wachezaji wa kukodi badala ya kujenga msingi wa kudumu.

6. Ushawishi Mdogo wa Kisiasa na Kijamii

Katika muktadha wa Tanzania, mafanikio ya baadhi ya vilabu yamechangiwa pia na ushawishi wa viongozi wakubwa serikalini au katika sekta binafsi. Toto Africans haikuwa na "msuli" huo wa kisiasa au kijamii ambao ungeisaidia kuvutia rasilimali.

7. Kutokuimarika Kwa Mapato ya Milango Mbadala.

Meneja wa Habari wa timu ya Yanga FC Ally Shaban Kamwe leo amegawa kadi kwa Wanachama wapya wa tawi la Maduka Manane Mwa...
03/08/2025

Meneja wa Habari wa timu ya Yanga FC Ally Shaban Kamwe leo amegawa kadi kwa Wanachama wapya wa tawi la Maduka Manane Mwanza ukiwa ni mikakati na kampeni ya Tofali la ubingwa 2025/2026.

Yanga imekuwa na mkakati wa kuongeza idadi ya Wanachama na mashabiki wa Klabu hiyo Ili waweze kuinua pato la timu katika sekta ya usajili na uendeshaji wa timu hiyo msimu mzima.

Sijui timu zingine zilizo ligi kuu NBC zinasemaje? Au ndio zimelala usingizi wa pono! Wakija kushtuka Yanga itakuwa na Wanachama Milioni 60. Na hapo ndio ubishi utaanza tena nani ana Wanachama na mashabiki wengi Tanzania?

Hongera sana Yanga, hongera Semaji na hongera Mkurugenzi wa Wanachama . Mnafanya kazi kubwa.

Feisal Salum Abadallah "Feitoto" | Mchezaji bora mechi ya ufunguzi Michuano ya Chan | Dar es Salaam.Kashacheza JKU✅Kasha...
03/08/2025

Feisal Salum Abadallah "Feitoto" | Mchezaji bora mechi ya ufunguzi Michuano ya Chan | Dar es Salaam.

Kashacheza JKU✅
Kashaceza Singida United✅
Kashacheza Yanga ✅
Kashacheza Azam FC ✅

Sasa ni zamu yake kucheza Simba SC
Kisha ataenda kucheza Soka nje ya Nchi.

Nani anabisha! Weka mzigo tu.

FT | Tanzania 2 - 0 Burkina Faso ⚽Abdul Suleiman Sopu ⚽ Mohamed Hussein ✍️Pointi tatu muhimu kwa Taifa Stars ✍️Mudathir ...
02/08/2025

FT | Tanzania 2 - 0 Burkina Faso

⚽Abdul Suleiman Sopu
⚽ Mohamed Hussein

✍️Pointi tatu muhimu kwa Taifa Stars
✍️Mudathir & Kagoma wamepewa kadi ya Njano

Nani man of the Match leo?
1. Feisal Salum
2. Mohamed Hussein
3. Clement Mzize
4. Yusuf Kagoma

Stars ikipata ushindi mechi ijayo inakuwa imejiweka nafasi nzuri kufuzu kwenda hatua inayofuata!!

Viva Taifa Stars
Viva Tanzania.

🌍📦 STAR EXPRESS CARGO."Mizigo kutoka China hadi Tanzania – Haraka, Salama, Kwa Uhakika!" 🇨🇳✈️🇹🇿Unanunua bidhaa China? Tu...
01/08/2025

🌍📦 STAR EXPRESS CARGO.

"Mizigo kutoka China hadi Tanzania – Haraka, Salama, Kwa Uhakika!" 🇨🇳✈️🇹🇿

Unanunua bidhaa China? Tuachie kazi ya usafirishaji!
Tunatoa huduma kamili kwa wafanyabiashara na wajasiriamali:

✅ Kununua bidhaa kwa niaba yako
✅ Kukusanya & kuunganisha mizigo
✅ Usafirishaji kwa bahari na ndege
✅ Ufuatiliaji wa mizigo hadi Tanzania
✅ Ushauri wa wauzaji wa kuaminika China
✅ Huduma kwa mteja kwa lugha ya Kiswahili

📞 Wasiliana Nasi:
🇨🇳 China: +86 175 7503 0095
🇹🇿 Tanzania: +255 713 581 614

📍 Makao Makuu: Guangzhou, China
广州市越秀区广元西路219号喀麦隆大厦 2楼 253

Room 253, 2nd Floor, Cameroon Building, No. 219 Guangyuan West Road, Yuexiu District, Guangzhou, china
📸 Instagram & Facebook: Star Express Cargo TZ

🛒 Usinunue kwa kubahatisha – fanya biashara na watu waaminifu!

📦 Star Express Cargo – Tunakuletea hadi mlangoni!

Baadhi ya Viongozi wa Simba SC wanahujumu timu yao. Kocha Fadlu alipendekeza Antony Mligo kutoka Namungo asajiliwe.Wao w...
30/07/2025

Baadhi ya Viongozi wa Simba SC wanahujumu timu yao. Kocha Fadlu alipendekeza Antony Mligo kutoka Namungo asajiliwe.

Wao wakaona asajiliwe Miraji Abdallah kutoka Coastal Union wakidhani Kocha akija atakubaliana na matakwa yao hayo.

Kocha Fadlu alipofika akashangaa kutokana na mtu ambaye hajapendekeza asajiliwe. Na akawauliza wakaanza aaaah aaaaha aaah.

Fadlu ameondoka leo na timu kwenda Misri na ameomba mchezaji huyu Antony Mligo akamilishiwe usajili wake na Ijumaa asafirishwe kwenda Egypt.

Kwa sababu hii kumbe baadhi ya Viongozi ndio kazi yao!! Anaambiwa na Kocha sajili huyu wewe unasajili wako! Ndio maana mnaabika.

Uoneni aibu hii sasa. Yani imebakia kuanza kuwataja hadharani warudisha mpira nyuma.

Kifupi mliohusika na hili mnaitwa VISHOKAAA!! BANDOKI haaaaaiii

HAPA atapigwa mtu k**a ngoma!! Amemisi mmoja pale Kati, namba 10 wa Taifa.Nani aanze 11, nani aanzie benchi?
30/07/2025

HAPA atapigwa mtu k**a ngoma!! Amemisi mmoja pale Kati, namba 10 wa Taifa.

Nani aanze 11, nani aanzie benchi?

Francis Baraza, raia wa Kenya, aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Biashara United Mara mwaka 2020.📊 TAKWIMU MUHIMU AKIWA BIAS...
30/07/2025

Francis Baraza, raia wa Kenya, aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Biashara United Mara mwaka 2020.

📊 TAKWIMU MUHIMU AKIWA BIASHARA UNITED (2020–2022):

🟢 MSIMU WA 2020/2021 – Ligi Kuu ya NBC Tanzania

Nafasi ya kumaliza ligi: 4

Alama (points): 55

Mechi zilizochezwa: 34

Ushindi: 15

Sare: 10

Kipigo: 9

Magoli yaliyofungwa: 37

Magoli waliyoruhusu: 27

✅ Hii ilikuwa mara ya kwanza Biashara kumaliza kwenye Top 4, ikiwapa nafasi ya kushiriki CAF Confederation Cup kwa mara ya kwanza kabisa.

🌍 CAF Confederation Cup 2021/22

Biashara United iliwakilisha Tanzania kwa mara ya kwanza kwenye michuano ya CAF.

Mchezo wa awali: Walicheza dhidi ya Dikhil FC kutoka Djibouti na kushinda jumla ya mabao 3-0.

Waliondolewa na Al Ahly Tripoli ya Libya katika raundi ya pili ya mtoano.

🔴 MSIMU WA 2021/2022

Mambo yalibadilika kwa kasi.

Biashara United ilianza vibaya ligi.

Baraza alifukuzwa kazi Februari 2022, baada ya matokeo mabaya mfululizo.

Wakati anaondoka, timu ilikuwa katika nafasi ya 14 kati ya 16 kwenye msimamo wa ligi.

💬 MAONI KUHUSU KAZI YAKE

Alijulikana kwa nidhamu, ufundishaji wa kisasa na kutumia vipaji vya wachezaji chipukizi.

Alisifiwa kwa kuibua nyota wa kusakata kabumbu bora kabisa.

Licha ya kuondolewa, alisaidia kuiweka Biashara United kwenye ramani ya soka la Afrika.

Na hii ni preseason tu....haziuzwiiiiiiii
30/07/2025

Na hii ni preseason tu....haziuzwiiiiiiii

LASSINE KOUMA | KARIBU JIJI LA MARAHA, ILA USIJE NA BEGI KUBWAK**ati ya usajili ya Klabu ya Yanga inaonekana kuwa na uan...
28/07/2025

LASSINE KOUMA | KARIBU JIJI LA MARAHA, ILA USIJE NA BEGI KUBWA

K**ati ya usajili ya Klabu ya Yanga inaonekana kuwa na uangalizi makini na mtazamo wa mbali katika kusaka vipaji. Ni dhahiri kuwa wameamua kusajili wachezaji wa kiwango cha juu, wenye uwezo wa kuleta tofauti uwanjani.

Miongoni mwa usajili mpya ni Lassine Kouma, raia wa Mali, ambaye sasa ni sehemu ya kikosi cha Wananchi. Ni mchezaji anayechukuliwa kwa matumaini makubwa, na tayari amepokea pongezi na matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wa soka nchini.

Kwa upande wangu binafsi, Kouma si jina kubwa kimataifa kwa sasa, japokuwa ana rekodi nzuri katika soka la kwao Mali. Nimepata fursa ya kutazama baadhi ya video zake kupitia YouTube, na bila shaka ana kipaji – ni “Mali” halisi kwa timu ya Yanga.

Hata hivyo, ni muhimu kutambua kuwa mafanikio katika soka la Tanzania yanahitaji zaidi ya kipaji pekee. Kuna haja ya kuwa na uvumilivu, kujituma, na uwezo wa kujibadilisha kulingana na mazingira ya hapa. Historia inaonyesha kwamba wapo wachezaji wengi wenye vipaji waliowahi kuja nchini, lakini wakashindwa kuendana na kasi au mazingira ya ligi ya Bongo.

Kwa mafanikio ya Kouma, itahitajika juhudi binafsi, nidhamu ya hali ya juu, na kuepuka vishawishi vya maisha ya starehe ambayo mara nyingi huwavuruga wachezaji wengi wageni.

Yanga wameonyesha nia, sasa ni zamu ya Kouma kuthibitisha ubora wake.

HAPA SIMBA SC MMEBUGI SANA | BAADAYE MSIANZE KULAUMUKupitia ukurasa rasmi wa Instagram wa Singida Black Stars, taarifa i...
27/07/2025

HAPA SIMBA SC MMEBUGI SANA | BAADAYE MSIANZE KULAUMU

Kupitia ukurasa rasmi wa Instagram wa Singida Black Stars, taarifa imetolewa kuwa Jonathan Sowah amesajiliwa rasmi na Simba SC. Mwanzoni, hizi zilionekana k**a tetesi zisizo na mashiko — lakini sasa ni rasmi. Hili, kwangu binafsi, si jambo la kushangaza.

Soka ni k**a siasa. Hakuna adui wa kudumu, wala rafiki wa kudumu. Lakini kuna baadhi ya matukio yanayozua maswali ya msingi.

Kabla ya kujiunga na Singida Black Stars, Sowah alipokuwa Medeama, alionekana wazi kuwa na mapenzi na heshima kubwa kwa Yanga SC. Aliposajiliwa na Singida, bado alikuwa na uhusiano wa karibu na miamba hao wa Jangwani. Hakuficha mapenzi yake kwa Yanga — hata Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said, alionekana kumwelewa na kumkubali.

Lakini leo, Sowah kasaini Simba SC. Swali ni, nini kilitokea kati ya Sowah na Hersi? Walikoseana wapi? Ni mazungumzo gani yalivunjika? Mambo haya hayapo wazi, lakini tunajua moja — mpango wa kumsajili Sowah Yanga umezimika, na Simba wamechukua nafasi hiyo.

Kumbuka: Huyu ni mchezaji ambaye alijiunga na Singida dirisha dogo la usajili, akasaidia timu hiyo kufuzu hadi Nusu Fainali ya CRDB Federation Cup, na pia akaipeleka Simba nje ya mashindano hayo! Leo hii huyo huyo amejiunga na Simba. Ajabu, siyo?

Inasemekana usajili huu umefanywa kwa ushawishi wa Mlezi wa Singida Black Stars, Mwigulu Nchemba, na Rais wa Simba, Mohamed Dewji. Je, hili ni tukio la mpango maalum au dili lililotengenezwa chini ya meza?

Wapo wanaosema kuwa Sowah ni chaguo la Kocha Fadlu Davids. K**a ni kweli, basi Fadlu anaamini anaweza kumrekebisha kiutendaji na kimaadili. Lakini je, Sowah ataweza kuendana na utamaduni wa soka la Kibongo? Ataweza kuhimili presha ya mashabiki, vyombo vya habari, na mahasimu wa jadi?

Tusisahau, kuna madai ya muda mrefu kwamba baadhi ya wachezaji hujihusisha na michezo ya kupanga matokeo — kuuza mechi! Siwezi kusema hili linamhusu Sowah, lakini kila tetesi ina chanzo chake. Wasiwasi ni kinga.

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports campaign tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports campaign tz:

Share

Category


Other Mwanza media companies

Show All